HEEE KUMBE BONGO MOVIE MWANZO MWISHO ULOZI!
COLETHA Raymond (PICHANI) mwigizaji wa
kike Bongo amefunguka kwa kusema kuwa tasnia ya filamu imetawaliwa na uchawi
kitu ambacho ni vigumu sana kuwaona baadhi ya wasanii kung’ara katika kazi za
sinema kwa sababu uchawi hauna ushahidi si rahisi kutamka hadharani.
“Wengi wanaogopa
kusutwa lakini lisemwalo lipo na kama halipo laja, suala la uchawi katika
tasnia ya filamu lipo wala watu wasikatae unakuta msanii anajua kuigiza lakini
kila sinema kapewa scene kidogo au hata akipewa nafasi kubwa haonekani
kafichwa,”anasema Coletha.
Msanii
huyo anataja baadhi ya wasanii ambao hadi leo wana uwezo mkubwa katika kuigiza
lakini hawaonekani hata ukikutana nao hawana hamu ya kuigiza tena kwani pamoja
na uwezo wao wa juu hawapewi nafasi wanaopewa nafasi ni wale waliojiweka sawa,
anawashauri waingiapo humo wajipange.
No comments:
Post a Comment