Sunday, December 21, 2014

PSPF YATOA MSADA WA MADAWATI BUYUNI II - CHANIKA, DAR ES SALAAM

Afisa Uhusiano mwandamizi wa Mfuko wa Pen sheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (Kushoto), akipena mikono na Ummy Shaaban, mwanafunzi wa darasa la sita shule ya msingi Buyuni II, iliyoko Chanika, wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam,wakati akikabidhi msada wa madawati kwa ajili ya shule hiyo mwishoni mwa wiki. (Katikati ni mwalimu mkuu wa shule hiyo, Rogather Palla.
Mwalimu Mkuu wa shule, Rogather Palla (Kulia), akitoa shukrani
Njaidi, (Kushoto), akitoa elimu kupitia vipeperushi kwa baadhi ya walimu wa shule hiyo
Wanafunzi wakibeba dawati kupeleka darasani

Ibada maalum ya kumuaga mch. M. Malekela - January 17, 2014. Karibuni wote!


Kikwete na mambo manne hukumu ya Escrow kesho

Kesho ni siku ya 23 kamili tangu Bunge litoe maazimio manane juu ya uwajibikaji wa wahusika wote katika kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 kutoka akaunti ya Tegeta Escrow, ambayo Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kutoa maamuzi yake, lakini akikabiliwa na mambo makuu manne.

Katika hukumu ambayo Rais Kikwete ataitoa kesho, suala la maazimio ya Bunge kuhusu kuwawajibisha viongozi waandamizi wa serikali ambao aliwateua, linatarajiwa kupata ufumbuzi.

Hawa ni pamoja na mawaziri, Profesa Sospeter Muhongo (Nishati na Madini); Profesa Anna Tibaijuka (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi.

Azimio la Bunge lilitamka wazi kwamba mamlaka ya uteuzi wao ambayo ni Rais Kikwete, atengue nafasi zao kutokana na kuhusika kwao katika kashfa hiyo.

RAIS JK ATUNUKU KAMISHENI KWA MAAFISA WAPYA WA JESHI

Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi na kumpongeza Luteni Usu Edwin Engelbert Kessy wakati wa hafla ya kutunuku kamisheni maafisa wa jeshi baada kuibuka mwanafunzi bora wakati wa mafunzo ya maafisa wa jeshi yaliyofanyika katika chuo cha jeshi Monduli mjini Arusha jana.
Rais Kikwete akitunuku Kamisheni maafisa wa jeshi katika chuo cha Jeshi huko Monduli Mkoani Arusha jana. Jumla ya maafisa 171 walitunukiwa kamisheni wakati wa hafla hiyo. (Picha na Freddy Maro.)

No comments:

Post a Comment