KENYA: MASENETA WA CORD WAPINGA MSWADA WA KUKABILI MAGAIDI
Na CHARLES WASONGA
MASENETA wa muungano wa Cord wamepinga Mswada unaolenga kubadilisha
sheria za sekta ya usalama nchini wakisema unahujumu haki za kikatiba za
raia.
Bw Moses Wetangula. Picha/MAKTABA
Wakiongozwa na Bw Moses Wetang’ula (Bungoma) viongozi hao walitaja
Mswada huo uliowasilishwa na serikali bungeni Jumanne kuwa dhalimu na
wakatisha kupeleka kesi kortini kupinga sheria hiyo iwapo Rais Uhuru
Kenyatta ataiidhinisha.
“Sisi kama viongozi hatuwezi kukubali Mswada kama huu ambao kimsingi
unaondoa haki za kibinadamu ambazo Wakenya walilipigania kwa zaidi ya
miongo miwili wakitetea Katiba hii ya sasa ambayo inalinda haki hizo.
Kisingizio kwamba hatua hiyo itasaidia vita dhidi ya ugaidi si kweli.
Watu wasio na hatia ndio wataumia zaidi,” Bw Wetang’ula akaambia
wanahabari kwenye majengo ya Bunge Jumatano.
Alisema kuzorota kwa usalama nchini kunasababishwa na uzembe wa vikosi
vya usalama na ufisadi wala sio kasoro katika sheria za usalama.
Maseneta wengine waliokuwa wameandamana naye ni Amos Wako (Busia, ODM),
Bonny Khalwale (Kakamega, UDF), James Orengo (Siaya), Johnstone Muthama
(Machakos, Wiper) na Mutula Kilonzo Junior (Makueni, Wiper).
“Mashambulizi ya Mandera na yale ya Mpeketoni yalitokana na uzembe wa
vikosi vya usalama. Ni wazi pia kwamba baadhi ya maafisa wa polisi
hupokea hongo kutoka kwa wahalifu, hasa magaidi, na hivyo kuwaruhusu
kupata nafasi ya kuwadhuru Wakenya,” akasema Bw Wetang’ula akitetea
pendekezo la magavana la kugatuliwa kwa sekta ya usalama.
Akiwasilisha Mswada huo, kiongozi wa wengi katika Bunge la Kitaifa Aden
Duale alisema una vipengee vinavyofanikisha juhudi za serikali za
kupambana na ugaidi, ambao umekuwa kero kubwa la usalama nchini.
Bw Duale alikuwa akizungumza kuhusu msururu wa mashambulizi ya kigaidi
ambayo yamesababisha ya Wakenya zaidi ya 64 katika Kaunti ya Mandera na
mafunzo ya itikadi za kigaidi kwenye misikiti eneo la Pwani.
Deni
Bw Orengo alisema Mswada huo pia utahujumu uhuru wa wanahabari kutokana
na kipengee kinachotoa adhabu kali dhidi ya uchapishaji na usambazaji wa
habari na picha zitakazofasiriwa kuwa za kueneza chuki na woga kwa
umma.
Wakati huo huo, maseneta hao walipinga hoja iliyopitishwa bungeni
Jumanne ambayo itaruhusu serikali kuongeza kiwango cha mkopo wa kigeni
kutoka Sh1.2 trilioni hadi Sh2.5 trilioni.
Wanataka hoja hiyo iwasilishwe katika Seneti ili ujadiliwe kwa kina wakisema hatua hiyo inahusu kaunti.
“Mzigo huu wa madeni utaathiri vibaya kiwango cha fedha zinazotengewa
serikali za kaunti. Isitoshe, pesa za kulipia madeni ya kigeni
zitatokana na ushuru wa Wakenya wote. Hii ndio maana suala hili linafaa
kuwasilishwa kwa Seneti,” akasema Bw
No comments:
Post a Comment