Wednesday, December 10, 2014

Makamu wa Rais Dkt. Bilal Ahutubia katika Mkutano wa 20 Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi Duniani (COP 20) Jiji la Lima Peru.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wenzake wakati walipohudhuria katika Mkutano wa 20 wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, unaoendelea Jijini Lima nchini Peru, ambapo  alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi. Pamoja na mambo mengine Dkt. Bilal alizungumzia namna nchi za Afrik zilivyojizatiti katika maazimio mbalimbali yanayolenga kunusuru majanga yatokanayo na Tabianchi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia katika Mkutano wa 20 wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, unaoendelea Jijini Lima nchini Peru. Makamu wa Rais alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi. Pamoja na mambo mengine Dkt. Bilal alizungumzia namna nchi za Afrika zilivyojizatiti katika maazimio mbalimbali yanayolenga kunusuru majanga yatokanayo na Tabianchi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mjumbe maalum wa Marekani katika masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi, Todd Stern, baada ya kuhudhuria katika Mkutano wa 20 wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, unaoendelea Jijini Lima nchini Peru, ambapo  alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi. Pamoja na mambo mengine Dkt. Bilal alizungumzia namna nchi za Afrika zilivyojizatiti katika
maazimio mbalimbali yanayolenga kunusuru majanga yatokanayo na Tabianchi. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipiga picha ya kumbukumbu na Mkuu wa Ujumbe wa China, katika mkutano wa Mkutano wa 20 wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Xie Zhenhua, wakati walipokutana kwa mazungumzo baada ya kuhudhuria na kuhutubia katika mkutano huo unaoendelea Jijini Lima nchini Peru, ambapo  alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi. Pamoja na mambo mengine Dkt. Bilal alizungumzia namna nchi za Afrik zilivyojizatiti katika maazimio mbalimbali yanayolenga kunusuru majanga yatokanayo na Tabianch
Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya Mawaziri wakati wakitoka katika chumba cha mkutano huo. Picha na OMR


Taarifa ya Vyombo vya Habari

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MHESHIMIWA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AMUWAKILISHA 

RAIS JAKAYA KIKWETE KWENYE MKUTANO WA MAZINGIRA 

(COP20) JIJINI LIMA, PERU DESEMBA 10, 2014
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal jana Desemba 09, 2014 amemuwakilisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ni Mwenyekiti Kamati ya Wakuu wa Nchi na Serikali Barani Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi, kwenye mkutano wa Kimataifa wa Mazingira Duniani (Cop20) unaofanyika jijini Lima, Peru.
Pamoja na shughuli nyingine ambazo zimemuhusisha Mheshimiwa Makamu wa Rais Dkt. Bilal katika Mkutano huo ikiwa pamoja na kuwa eneo la Mazingira nchini liko chini ya Ofisi yake, Mheshimiwa Dkt, Bilal alipata fursa ya kutoa hotuba kwa niaba ya Wakuu wa Nchi za Afrika siku ya Ufunguzi wa Mkutano huo, huku akisisitiza katika hotuba hiyo umuhimu wa kila nchi kushiriki katika kukabiliana na hali ya mabadiliko ya tabia nchi na tena akaelezea kuwa, hakuna anayeweza kupona kwa kujificha ama kuachia kazi hii ifanywe na nchi baadhi na akaongeza kuwa, wanaochangia kwa kasi kubwa kuathiri mazingira wanatakiwa 
kutambua kwamba wanayoyafanya hayatawanufaisha milele hivyo nao washiriki kwa vitendo katika kukabiliana na janga hili kubwa linaloikumba dunia kwa sasa.
Awali akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon alieleza kuwa yapo mabadiliko ya tabia nchi ambayo kimsingi yametengenezwa na binadamu wenyewe na kama binadamu wakiamua kukabiliana nayo 
wanaweza kabisa kuyatokomeza. Pia alifafanua kuhusu nadharia ya nchi kushirikiana kwa kuwa mabadiliko haya kwa sasa athari zake hazina mipaka na kwamba nchi zote lazima ziwe katika sehemu ya utatuzi wa tatizo hili kubwa linaloikabili dunia.
“Tutumie mapendekezo ya Lima kufungua njia mpya, tuwe na vipaumbele vinavyotekelezeka na kuonekana, Tutoke hapa Lima na twende kuandika historia mpya kwa dunia yetu,” alimalizia Ban Ki-moon.
Kwa upande wa Rais wa mkutano huo (Cop20) Manuel Pulgar-Vida ambaye pia ni Waziri wa Mazuingira wa Peru, alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha washiriki wa mkutano huo nchini Peru kwa niaba ya Rais wa nchi hiyo Mheshimiwa Olanta Humala na kisha akafafanua kuwa nchi ya Peru imepitia masaibu kadhaa ya kimazingira na hivyo kupata nafasi ya kuandaa mkutano huu kwao ni heshima na wajibu katika dunia na kwamba anategemea maazimio ya Lima yasaidie dunia katika kukab iliana na tatizo hili 
linalokuwa la mabadiliko ya tabia nchi.
Kauli ya Mheshimiwa Manuel Pulgar inasadifu ile aliyoitoa pia  Christiana Fugueres, Katibu Mtendaji wa Umoja wa Mataifa wa Mkakati wa kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia Nchi ambaye aliuambia mkutano huo kuwa, wakati umefika kwa nchi zote kukabiliana na matatizo ya mabadiliko ya tabia nchi kwa pamoja kwa kuwa yanachangia kuongeza umaskini na ili jamii ipate ahueni, basi ni wajibu kwa kila binadanmu kuchukua nafasi yake katika kukabiliana na hali hii iliyopo.
Katika tukio jingine, Mheshimiwa Makamu wa Rais alipata fursa ya kukutana na Ujumbe kutoka Marekani uliongozwa na Mjumbe Maalum kutoka Serikali ya Marekani anayehusika na masuala ya Mabadiliko ya Tabia nchi Todd Stern, ambaye alimueleza Mheshimiwa Makamu wa Rais kuhusu utayari wa serikali ya Marekani katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na kwamba nchi yake itashirikiana nan chi zinazoendelea ikiwemo Tanzania katika suala hilo.
 Vile vile Mheshimiwa Makamu wa Rais alipata nafasi ya kukutana na ujumbe kutoka Jamhuri ya Watu wa China ulioongozwa na Mheshimiwa Xie Zhenhua ambaye alizungumzia kuhusu ushirikiano baina ya nchi zinazoendelea na zile zilizoendelea katika suala la mabadiliko ya tabia nchi na akafafanua kuwa Tanzania na China zina uhusiano wa kindugu hivyo kama kutakuwa na jambo la kipekee baina ya nchi hizi mbili basi serikali ya China iko wazi kulipokea.

Rais Kikwete atunuku nishani za miaka 50 ya Uhuru

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein (kutoka kushoto) Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi (katikati) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda wakiwa  hafla kutunuku nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano iliyofanyika  viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la pili Augustino Stephene Ramadhan katika hafla kutunuku nishani katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la pili Ali Salum Ahmed katika hafla kutunuku nishani katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la pili Mohammed Fakih Mohammed katika hafla kutunuku nishani katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la tatu Amani Issack Abraham Sepetu kwa niaba ya Baba yake Issack Abraham Sepetu (marehemu) katika hafla kutunuku nishani katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la tatu Ali Ameir Mohamed katika hafla kutunuku nishani iliyofanyika  viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la nne Haji Machano  Haji  katika hafla kutunuku nishani iliyofanyika  viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na Ikulu.]

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku nishani ya miaka 50 ya Muungano daraja la nne Bibi Johari Yussufu Akida katika hafla kutunuku nishani iliyofanyika  viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam sambamba na maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana.[Picha na
Sophie Mbeyu Blog twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail WELCOME SOPHIE MBEYU BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: +460762898798 | Email: sophiambeyu@msn.com | KARIBU SOPHIE MBEYU BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: +460762898798 | Barua Pepe: sophiembeyu@msn.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA Home About Products LIVE TV Radio Contact Wednesday, 10 December 2014 BAADA YA KUPAMBANA NA JAMBAZI MUUZA CHIPSI APEWA NISHANI NA RAIS KIKWETE Rais Jakaya Kikwete jana aliwatunuku nishani Watanzania 28, akiwamo muuza chips, Kassim Said Kassim (28), ambaye aliyepewa nishani na ushupavu baada ya kupambana na kumdhibiti jambazi mwenye silaha. Hafla ya utoaji wa nishani hizo ilifanyika jana jioni katika Viwanja vya Ikulu na kuhudhuriwa na mabalozi na viongozi mbalimbali wa Serikali, huku Kassim akiwa kivutio kutokana na idadi kubwa ya watu kushangazwa na ujasiri wake wa kupambana na jambazi mwenye silaha. Kijana huyo alikuwa wa mwisho kutajwa na baada ya mshereheshaji wa hafla hiyo kueleza historia yake kwa kifupi kwamba alizaliwa mwaka 1986, iliibuka miguno kutoka kwa wageni waliohudhuria hafla hiyo na aliposimulia kisa chenyewe, kila mtu aliduwaa. Baadaye Kassim alimweleza mwandishi wetu: “Nilikuwa nafanya biashara ya chips eneo la Buguruni Malapa. Nakumbuka Julai 7, mwaka jana saa tatu usiku tulivamiwa na jambazi aliyekuwa na bastola na kuanza kuwatishia wateja, akitaka kupatiwa fedha na vitu mbalimbali. “Kwanza alianza kuwashinikiza wateja wampatie fedha na alipoona hakuna aliyemsikiliza, alichomoa bastola na kumtishia mmoja wa wateja, hapo ndipo nilipoamua kupambana naye.” Alisema alichukua chepe na kumpiga nalo mara mbili sehemu ya kichwani hadi alipoanguka na kuzirai. Alisema baada ya hapo, alitoa ripoti polisi ambao walifika na kumchukua. Viongozi waliotunukiwa Nishani ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Muungano Daraja la Pili ni Adam Sapi Mkwawa (marehemu), Erasto Man’genya (marehemu), Pius Msekwa, Samuel Sitta, Francis Nyalali (marehemu), Augustino Ramadhani, Timoth Apiyo (marehemu), Paul Rupia, Ali Salum Ahmed na Mohammed Fakih Mohammed. Waliopewa Nishani ya Kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano Daraja la Tatu ni Peter Kisumo, Anna Abdallah, Kingunge Ngombare-Mwiru, Isaack Sepetu (marehemu), Alli Mzee Alli (marehemu), Brigedia Jenerali mstaafu Adam Mwakanjuki (marehemu). Ali Ameir Mohamed, Al-Noor Kassum, Jenerali mstaafu Ernest Kiaro (marehemu), Solomon Liani (marehemu), Augustine Mahiga, Phillemon Mgaya, Ambindwile Mwaijande (marehemu) na Simeon Mwanguku. Waliopewa Nishani ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Muungano Daraja la Nne ni Sophia Kawawa (marehemu), Haji Machano Haji, Johari Yusufu Akida na Bendi ya Atomic Jazz. Jenerali mstaafu David Musuguri alipewa Nishani ya Operesheni Safisha Msumbiji huku Kassim akipewa nishani ya ushupavu. Chanzo: Mwananchi Posted by Sophia Mbeyu at 17:15 Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest No comments: Post a Comment Links to this post Create a Link Newer Post Older Post Home Translate Powered by Translate PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA UNAHITAJI BOFYA PICHA HII KUONA PICHA ZAIDI About Me My Photo Sophia Mbeyu View my complete profile Blog Archive Popular Posts MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2014 YAMETOKA, INGIA HUMU KUONA DK. CHARLES E. MSOND E AKITANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MAPEMA HII LEO OFISINI KWAKE,MSONDA AMESEMA MATOKEO YA MWAKA HUU UFAURU WAKE ... MITINDO YA VITENGE KWA WANAWAKE NA WANAUME... KAMA INAVYYONYESHA PICHA! VAZI LAKITENGE LAWEZA KUTUMIWA KAMA VAZI LA OFISI AMA CASUAL SIO LAZIMA KITENGE KIWE N... MITINDO YA VITENGE KWA AKINA DADA NA WATOTO.. MITINDO MBALIMBALI YA VITENGE, VIATU NA HANDBAG ZA KITENGE.... MITINDO YA VITENGE,VIATU, MIKUFU KWA AJILI YA SHEREHE MAALUM! MITINDO YA VITENGE HII NI SKIRT ILIYOSHONWA KWA KITENGE! KAMA TULIVYOONA SASA HIVI VITENGE SIYO TU MAGAUNI HATA SKIRT, SURUALI NA E.T.C... AKINA B... MITINDO BOMBA YA VITENGE! Huhitaji nguo za majina kupendeza, kitu cha kitenge tosha kabisa kukutoa bomba! MITINDO MBALIMBALI YA VITENGE..... MITINDO YA VITENGE Mitindo ya Vitenge inaweza kushonwa katika dizain mbalimbali, hii inaonyesha mitindo kwa vijana ni katika kuonyesha kuwa kitenge si lazima ... MITINDO YA VITENGE KWA WOTE,.... WADAU WA VITENGE KILA WIKI KUNA POST YA VITENGE FUATILIA POST ZA NYUMA KUPATA MITINDO MBALIMBALI ZAIDI... Labels African day 2008 may AMUUA BABA YAKE KUMUOKOA SHANGAZI YAKE ALIYEKUWA ANABAKWA- NACHINGWEA ARIEL SHARON AFARIKI ASEMA YADHOOFISHA UCHUMI AFRIKA aswira Kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar:Rais wa Comoro Awasili Zanzibar Kuhudhuria Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi BAADA YA BASI KUGONGA NA KUUA WATATU BABA NA MWANA JAY-Z NA MWANAE BLUE IVY.. Biza mupulu artist Biza mupulu Botswana BREAKING NEWS: FIFA YAHAMISHA MUDA WA KOMBE LA DUNIA MWAKA 2022 HUKO QATAR HABARI ZA KIMATAIFA/ WAUMINI WAUAWA MSIKITINI NCHINI NIGERIA HABARI ZA UMBEYA/. WAKATI WEMA AKITUMA VIDEO YA DIAMOND AKIWA KITANDANI HAKUNA KAMA MWANAMKE HAPO NAPO SASA IGP ATANGAZA MABADILIKO MAKUBWA JESHI LA POLISI. IJUMAA NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG.... IMETANGAZWA RASMI KESHO NI SIKU YA MAPUMZIKO KUSHEHEREKEA MAPINDUZI: Kundi la FM Academia KUTWAA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA NJE YA AFRIKA Machael Jackson kuaga dunia MADAWA YA KULEVYA YAINGIZWA SUPERMARKET KATIKA MAKASHA YA NDIZI MAGAZETI YA LEO IJUMAA 10 JANUARY 2014 Magonjwa ya mlipuko yanukia jijini Dar MAN UNITED YAZINDUKA Mariam bongo MAWAZIRI WAPYA WATANO WATAJWA TANZANIA MITINDO YA NYWELE MITINDO YA VITENGE MKAPA AIPONDA MISAADA KUTOKA NJE MSIKIE JOKATE AKIONGELEA MUZIKI NA FILAMU....... Mwekezaji abomoa nyumba za wananchi wa Mkuyuni-Morogoro ili kupisha ujenzi wa Majosho.11 jan mgogoro Nondoz wa Bongo waliokamilisha kisomo chao Data India. Pablo Machine Familia dar Pablo Machine na watoto Pablo Machine na wakenya kwenye festival Pablo Machine Sabiti PENNY NAE ANENA "HAITATOKEA KAMWE NIKAMDHARAU DIAMOND PICHA ZA WATUHUMIWA WALIOKAMATWA WAKISAFIRISHA SILAHA ZA KIVITA KATAVI PICTURE OF THE DAY..KWA RAHA ZAO Rais wa Zanzibar Dr Ali Shein Aendelea Kutunuku Nishani Rihanna out in Barbados RWANDA YAKANUSHA UVUMI KUHUSU KIFO CHA KAGAME SABABU YA KIFO CHA MPENDWA WETU ZAINAB BUZOHERA TASWIRA MBALI MBALI KATIKA SHEREHE YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI ZANZIBAR LEO 12/01/2014 UNAKANDAMIZA ... VAZI LA LEO Wa Bongo WAFANYABIASHARA WA DAR WAGOMEA MASHINE ZA KODI ZA TRA WAFUNGA MADUKA LEO Wakali bongo hawo WANANCHI WALITEKETEZA BASI KWA MOTO WAZIRI KIGODA : MFUMO MASHINE EFDs NI MBOVU WEEKEND NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG....NAWAPENDAAA MINGIIII. WEMA NI MAMA KIJACHO? SOMA ALICHOANDIKA HAPO Wizara ya maliasili na utalii imewasimamisha kazi watumishi wake 22 wa idara ya wanyama pori YAICHAPA 2-0 SWANSEA CITY Yatima Dar walilia madarasa yakujisomea PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE powered by Slideshow Sikiliza clouds radio SIKILIZA KWANZA JAMII RADIO Followers Google+ Followers Total visitors Total Pageviews Sparkline 1278904 CLOCK & CALENDAR buy research paper custom essay writing answering service care December 2014 S M T W T F S 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 Free Counter Counter Free PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE WEBSITES & BLOGS MICHUZI JIACHIE BONGOBLOGS TanzMED Wavuti Allyshams Myummah76 Francis Godwin Globalpublishers Full Shangwe Ladyjaydee Swahili TV TMF Haki Ngowi Mimi na Tanzania Mo Blog Chadema Blog CCM Blog January Makamba Zitto kabwe Habari Leo Daily News Mwananchi Mtanzania Tanzania Daima Raia Mwema Majira Mwanaspoti The Citizen Daraja Letu IPP Media Bashir Nkoromo BBC Swahili Sauti ya Amerika Jamii Forums BLOG DEVELOPMENT BLOG DEVELOPMENT AUDIO BAR SIKILIZA BRAND NEW TRACK HAPA!! VIDEO BAR UNATAKA KUPUNGUA UZITO!! CLICK THIS IMAGE Contact Form Name Email * Message * TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA UNAHITAJI BOFYA PICHA HII KUONA PICHA ZAIDI UNAHITAJI KUPUNGUA UZITO WEIGHT MANAGEMENT UNAHITAJI KIKAPU UNAHITAJI KIKAPU SANDALS SANDALS ADVERTISE WITH US PLACE YOUR ADS HERE AFRICAN FASHION TANGAZO BOFYA! Copyright (c) 2007 Sophie Mbeyu Blog | Maintained By ALLY S MGIDO'S +255657615174

Make Money at : http://bit.ly/copy_win
Sophie Mbeyu Blog twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail WELCOME SOPHIE MBEYU BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: +460762898798 | Email: sophiambeyu@msn.com | KARIBU SOPHIE MBEYU BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: +460762898798 | Barua Pepe: sophiembeyu@msn.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA Home About Products LIVE TV Radio Contact Wednesday, 10 December 2014 BAADA YA KUPAMBANA NA JAMBAZI MUUZA CHIPSI APEWA NISHANI NA RAIS KIKWETE Rais Jakaya Kikwete jana aliwatunuku nishani Watanzania 28, akiwamo muuza chips, Kassim Said Kassim (28), ambaye aliyepewa nishani na ushupavu baada ya kupambana na kumdhibiti jambazi mwenye silaha. Hafla ya utoaji wa nishani hizo ilifanyika jana jioni katika Viwanja vya Ikulu na kuhudhuriwa na mabalozi na viongozi mbalimbali wa Serikali, huku Kassim akiwa kivutio kutokana na idadi kubwa ya watu kushangazwa na ujasiri wake wa kupambana na jambazi mwenye silaha. Kijana huyo alikuwa wa mwisho kutajwa na baada ya mshereheshaji wa hafla hiyo kueleza historia yake kwa kifupi kwamba alizaliwa mwaka 1986, iliibuka miguno kutoka kwa wageni waliohudhuria hafla hiyo na aliposimulia kisa chenyewe, kila mtu aliduwaa. Baadaye Kassim alimweleza mwandishi wetu: “Nilikuwa nafanya biashara ya chips eneo la Buguruni Malapa. Nakumbuka Julai 7, mwaka jana saa tatu usiku tulivamiwa na jambazi aliyekuwa na bastola na kuanza kuwatishia wateja, akitaka kupatiwa fedha na vitu mbalimbali. “Kwanza alianza kuwashinikiza wateja wampatie fedha na alipoona hakuna aliyemsikiliza, alichomoa bastola na kumtishia mmoja wa wateja, hapo ndipo nilipoamua kupambana naye.” Alisema alichukua chepe na kumpiga nalo mara mbili sehemu ya kichwani hadi alipoanguka na kuzirai. Alisema baada ya hapo, alitoa ripoti polisi ambao walifika na kumchukua. Viongozi waliotunukiwa Nishani ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Muungano Daraja la Pili ni Adam Sapi Mkwawa (marehemu), Erasto Man’genya (marehemu), Pius Msekwa, Samuel Sitta, Francis Nyalali (marehemu), Augustino Ramadhani, Timoth Apiyo (marehemu), Paul Rupia, Ali Salum Ahmed na Mohammed Fakih Mohammed. Waliopewa Nishani ya Kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano Daraja la Tatu ni Peter Kisumo, Anna Abdallah, Kingunge Ngombare-Mwiru, Isaack Sepetu (marehemu), Alli Mzee Alli (marehemu), Brigedia Jenerali mstaafu Adam Mwakanjuki (marehemu). Ali Ameir Mohamed, Al-Noor Kassum, Jenerali mstaafu Ernest Kiaro (marehemu), Solomon Liani (marehemu), Augustine Mahiga, Phillemon Mgaya, Ambindwile Mwaijande (marehemu) na Simeon Mwanguku. Waliopewa Nishani ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Muungano Daraja la Nne ni Sophia Kawawa (marehemu), Haji Machano Haji, Johari Yusufu Akida na Bendi ya Atomic Jazz. Jenerali mstaafu David Musuguri alipewa Nishani ya Operesheni Safisha Msumbiji huku Kassim akipewa nishani ya ushupavu. Chanzo: Mwananchi Posted by Sophia Mbeyu at 17:15 Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest No comments: Post a Comment Links to this post Create a Link Newer Post Older Post Home Translate Powered by Translate PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA UNAHITAJI BOFYA PICHA HII KUONA PICHA ZAIDI About Me My Photo Sophia Mbeyu View my complete profile Blog Archive Popular Posts MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2014 YAMETOKA, INGIA HUMU KUONA DK. CHARLES E. MSOND E AKITANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MAPEMA HII LEO OFISINI KWAKE,MSONDA AMESEMA MATOKEO YA MWAKA HUU UFAURU WAKE ... MITINDO YA VITENGE KWA WANAWAKE NA WANAUME... KAMA INAVYYONYESHA PICHA! VAZI LAKITENGE LAWEZA KUTUMIWA KAMA VAZI LA OFISI AMA CASUAL SIO LAZIMA KITENGE KIWE N... MITINDO YA VITENGE KWA AKINA DADA NA WATOTO.. MITINDO MBALIMBALI YA VITENGE, VIATU NA HANDBAG ZA KITENGE.... MITINDO YA VITENGE,VIATU, MIKUFU KWA AJILI YA SHEREHE MAALUM! MITINDO YA VITENGE HII NI SKIRT ILIYOSHONWA KWA KITENGE! KAMA TULIVYOONA SASA HIVI VITENGE SIYO TU MAGAUNI HATA SKIRT, SURUALI NA E.T.C... AKINA B... MITINDO BOMBA YA VITENGE! Huhitaji nguo za majina kupendeza, kitu cha kitenge tosha kabisa kukutoa bomba! MITINDO MBALIMBALI YA VITENGE..... MITINDO YA VITENGE Mitindo ya Vitenge inaweza kushonwa katika dizain mbalimbali, hii inaonyesha mitindo kwa vijana ni katika kuonyesha kuwa kitenge si lazima ... MITINDO YA VITENGE KWA WOTE,.... WADAU WA VITENGE KILA WIKI KUNA POST YA VITENGE FUATILIA POST ZA NYUMA KUPATA MITINDO MBALIMBALI ZAIDI... Labels African day 2008 may AMUUA BABA YAKE KUMUOKOA SHANGAZI YAKE ALIYEKUWA ANABAKWA- NACHINGWEA ARIEL SHARON AFARIKI ASEMA YADHOOFISHA UCHUMI AFRIKA aswira Kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar:Rais wa Comoro Awasili Zanzibar Kuhudhuria Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi BAADA YA BASI KUGONGA NA KUUA WATATU BABA NA MWANA JAY-Z NA MWANAE BLUE IVY.. Biza mupulu artist Biza mupulu Botswana BREAKING NEWS: FIFA YAHAMISHA MUDA WA KOMBE LA DUNIA MWAKA 2022 HUKO QATAR HABARI ZA KIMATAIFA/ WAUMINI WAUAWA MSIKITINI NCHINI NIGERIA HABARI ZA UMBEYA/. WAKATI WEMA AKITUMA VIDEO YA DIAMOND AKIWA KITANDANI HAKUNA KAMA MWANAMKE HAPO NAPO SASA IGP ATANGAZA MABADILIKO MAKUBWA JESHI LA POLISI. IJUMAA NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG.... IMETANGAZWA RASMI KESHO NI SIKU YA MAPUMZIKO KUSHEHEREKEA MAPINDUZI: Kundi la FM Academia KUTWAA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA NJE YA AFRIKA Machael Jackson kuaga dunia MADAWA YA KULEVYA YAINGIZWA SUPERMARKET KATIKA MAKASHA YA NDIZI MAGAZETI YA LEO IJUMAA 10 JANUARY 2014 Magonjwa ya mlipuko yanukia jijini Dar MAN UNITED YAZINDUKA Mariam bongo MAWAZIRI WAPYA WATANO WATAJWA TANZANIA MITINDO YA NYWELE MITINDO YA VITENGE MKAPA AIPONDA MISAADA KUTOKA NJE MSIKIE JOKATE AKIONGELEA MUZIKI NA FILAMU....... Mwekezaji abomoa nyumba za wananchi wa Mkuyuni-Morogoro ili kupisha ujenzi wa Majosho.11 jan mgogoro Nondoz wa Bongo waliokamilisha kisomo chao Data India. Pablo Machine Familia dar Pablo Machine na watoto Pablo Machine na wakenya kwenye festival Pablo Machine Sabiti PENNY NAE ANENA "HAITATOKEA KAMWE NIKAMDHARAU DIAMOND PICHA ZA WATUHUMIWA WALIOKAMATWA WAKISAFIRISHA SILAHA ZA KIVITA KATAVI PICTURE OF THE DAY..KWA RAHA ZAO Rais wa Zanzibar Dr Ali Shein Aendelea Kutunuku Nishani Rihanna out in Barbados RWANDA YAKANUSHA UVUMI KUHUSU KIFO CHA KAGAME SABABU YA KIFO CHA MPENDWA WETU ZAINAB BUZOHERA TASWIRA MBALI MBALI KATIKA SHEREHE YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI ZANZIBAR LEO 12/01/2014 UNAKANDAMIZA ... VAZI LA LEO Wa Bongo WAFANYABIASHARA WA DAR WAGOMEA MASHINE ZA KODI ZA TRA WAFUNGA MADUKA LEO Wakali bongo hawo WANANCHI WALITEKETEZA BASI KWA MOTO WAZIRI KIGODA : MFUMO MASHINE EFDs NI MBOVU WEEKEND NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG....NAWAPENDAAA MINGIIII. WEMA NI MAMA KIJACHO? SOMA ALICHOANDIKA HAPO Wizara ya maliasili na utalii imewasimamisha kazi watumishi wake 22 wa idara ya wanyama pori YAICHAPA 2-0 SWANSEA CITY Yatima Dar walilia madarasa yakujisomea PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE powered by Slideshow Sikiliza clouds radio SIKILIZA KWANZA JAMII RADIO Followers Google+ Followers Total visitors Total Pageviews Sparkline 1278904 CLOCK & CALENDAR buy research paper custom essay writing answering service care December 2014 S M T W T F S 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 Free Counter Counter Free PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE WEBSITES & BLOGS MICHUZI JIACHIE BONGOBLOGS TanzMED Wavuti Allyshams Myummah76 Francis Godwin Globalpublishers Full Shangwe Ladyjaydee Swahili TV TMF Haki Ngowi Mimi na Tanzania Mo Blog Chadema Blog CCM Blog January Makamba Zitto kabwe Habari Leo Daily News Mwananchi Mtanzania Tanzania Daima Raia Mwema Majira Mwanaspoti The Citizen Daraja Letu IPP Media Bashir Nkoromo BBC Swahili Sauti ya Amerika Jamii Forums BLOG DEVELOPMENT BLOG DEVELOPMENT AUDIO BAR SIKILIZA BRAND NEW TRACK HAPA!! VIDEO BAR UNATAKA KUPUNGUA UZITO!! CLICK THIS IMAGE Contact Form Name Email * Message * TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA UNAHITAJI BOFYA PICHA HII KUONA PICHA ZAIDI UNAHITAJI KUPUNGUA UZITO WEIGHT MANAGEMENT UNAHITAJI KIKAPU UNAHITAJI KIKAPU SANDALS SANDALS ADVERTISE WITH US PLACE YOUR ADS HERE AFRICAN FASHION TANGAZO BOFYA! Copyright (c) 2007 Sophie Mbeyu Blog | Maintained By ALLY S MGIDO'S +255657615174

Make Money at : http://bit.ly/copy_win

Balozi Seif Atembelea Jengo la Maabara Kuu Mombasa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa na mwenyeji wake Mrajisi wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Dr. Burhan Othman Simai akikagua Maabara ya Bodi hiyo iliyopo kwenye jengo lao jipya   liliopo Mtaa wa Mombasa nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Mrajisi wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Dr. Burhan Othman Simai akimpatia maelezo Balozi Seif juu ya juhudi wanazochukuwa watendaji wa Bodi hiyo kukagua bidhaa mbali mbali zinazoingizwa nchini ili kujua ubora wake.
Mratibu wa mradi wa EAC – MRH ulio chini ya Bodi ya Chakula na Dawa Zanzibar Bibi Hidaya Juma akitoa maelezo ya maendeleo ya mrtadi huo mbele ya Balozi Seif aliyefika katika  Jengo la Bodi hiyo kulikagua.Kushoto ni Mrajisi wa Bodi ya Chalkula na Dawa Dr. Burhan Othman Simai.
Meneja wa Kitengo chaMtandao wa mawasiliano ya Kompyuta  cha Bodi ya Chakula na Dawa { ZFDB } Ndugu Mohamed Yahya Said aliyevaa shati rangi ya buluu akielezea mfumo wa Mradi wa MRH unaotoa fursa kwa Bodi ya Chakula na Dawa kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja ya mamlaka za Bodi nyengine Duniani.(Picha na Hassan Issa OMPR)

Balozi Seif Atembelea Jengo la Maabara Kuu Mombasa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa na mwenyeji wake Mrajisi wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Dr. Burhan Othman Simai akikagua Maabara ya Bodi hiyo iliyopo kwenye jengo lao jipya   liliopo Mtaa wa Mombasa nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Mrajisi wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Dr. Burhan Othman Simai akimpatia maelezo Balozi Seif juu ya juhudi wanazochukuwa watendaji wa Bodi hiyo kukagua bidhaa mbali mbali zinazoingizwa nchini ili kujua ubora wake.
Mratibu wa mradi wa EAC – MRH ulio chini ya Bodi ya Chakula na Dawa Zanzibar Bibi Hidaya Juma akitoa maelezo ya maendeleo ya mrtadi huo mbele ya Balozi Seif aliyefika katika  Jengo la Bodi hiyo kulikagua.Kushoto ni Mrajisi wa Bodi ya Chalkula na Dawa Dr. Burhan Othman Simai.
Meneja wa Kitengo chaMtandao wa mawasiliano ya Kompyuta  cha Bodi ya Chakula na Dawa { ZFDB } Ndugu Mohamed Yahya Said aliyevaa shati rangi ya buluu akielezea mfumo wa Mradi wa MRH unaotoa fursa kwa Bodi ya Chakula na Dawa kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja ya mamlaka za Bodi nyengine Duniani.(Picha na Hassan Issa OMPR)

No comments:

Post a Comment