Sunday, December 7, 2014

DIAMOND AMWIMBIA SHABIKI WAKE WIMBO WA SIKU YA KUZALIWA

Diamond Platnumz akimwimbia shabiki wake Osama Mwita kutoka Tanzania  wimbo wa siku ya kuzaliwa siku ya Jumamosi Desemba 6, 2014 kwenye sherehe ya Uhuru ilizofanyika katika hotel ya Sheraton Downtown Silver Spring, Maryland nchini Marekani.
Diamond akiendelea kumwimbia shabiki wake huyo ambaye usiku wa Desemba 6, 2014 ilikua ni siku yake ya kuzaliwa.

Mmoja ya mdau aliyenogesha urembo kwenye kucha kwa kuweka rangi ya kucha ya bendera ya Tanzania kwenye sherehe ya Uhuru DMV siku ya Jumamosi Desemba 6, 2014 iliyofanyika Sheraton ya Silver Spring, Maryland

MKUTANO WA KAMATI MAALUM YA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA (NEC)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai alipowasili katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja katika Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM alipowasili katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja katika Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Balozi Seif Ali Iddi (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai (kulia) wakiwa katika kikao cha siku moja cha Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.
Wajumbe wa Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) wakiwa katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja ulipofanyika mkutano huo leo chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.
Wajumbe wa Sekretarieti wa Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja wakiwa tayari kuweka kumbu kumbu kwa mabo yote yatakayozungumzwa katika Mkutano huo uliofanyika leo chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akitoa taarifa kwa Wajumbe wa Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ya (NEC) katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja kiako hicho kilifanyika leo chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Balozi Seif Ali Iddi (kushoto). Picha na Ikulu.


MAHAFALI YA 5 YA CHUO KIKUU KIKUU CHA ST, JOHN DODOMA YAFANA.

Mkuu wa chuo kikuu kikuu cha St, John Askofu Dolnad Mtetemela katikati akiwa na viongozi wa kanisa la anglikan ambalo ndilo mmiliki wa chuo hicho walipokuwa kwenye mahafali ya tano ya chuo hicho.
 Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Philip Alfred aliyekuwa Mgeni Rasmi kwenye mahafali ya tano ya wanafunzi wa chuo kikuu cha St, John's cha mjini Dodoma akihuwahutubia wahitimu wa kozi mbalimbali wa chuo hicho.
 Mkuu wa Skuli za kidini akihutubia jambo kwenye mahafali hayo.
Wahitimu wa Shahada ya sayansi katika uuguzi wakila kiapo cha utumishi uliotukuka wakati wa mahafali ya tano ya chuo kikuu cha St, John's kinachomilikiwa na kanisa la anglican kilichopo mjini Dodoma
Meneja wa CRDB Tawi la Dodoma Bi Rehema Hamisi akiwa na mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kukabidhi kwa viongozi wa chuo kikuu cha st, John's kama mchango wa maendeleo ya chuo hicho
kwa picha zaidi bofya soma zaidi

Rais Kikwete afanya Kisomo Kumshukuru Mwenyezi Mungu Kwa Kupona

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimia baadhi ya Mashekhe na wageni waliohudhuria hafla ya kisomo maalum cha Kumshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kufanyiwa upasuaji na kurejea nyumbani salama kilichofanyika katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam leo Jumapili Desemba 7, 2014.
Mjukuu wa Rais, Ayman Ridhiwani Kikwete akicheza kwa furaha wakati Babu yake Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwashukuru wageni na Mashekhe waliohudhuria hafla ya kisomo maalum kilichofanyika katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam leo Jumapili Desemba 7, 2014
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mjukuu wake Ayman Ridhiwani Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kumalizika kisomo cha shukran kwa Mwenyezi Mungu kiklichofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo Jumapili Desemba 7, 2014.(picha na Freddy Maro)

VIVAZI VYA RED CARPET SHEREHE YA UHURU DMV

Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

No comments:

Post a Comment