Membe achukua tahadhari ya escrow
Bagamoyo. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard
Membe amezindua mfuko wa elimu wa kusomesha wanafunzi waliofaulu kwenda
vyuo vikuu lakini familia zao hazina uwezo katika Chuo Kikuu cha
Bagamoyo (UB) huku akichukua hadhari dhidi ya kupokea “fedha kama zile
za Akaunti ya Tegeta Escrow”.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.PICHA|MAKTABA
Akiutangaza mfuko huo utakaojulikana kwa jina la ‘Bernard Membe Scholarship, waziri huyo aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya chuo hicho, alisema fedha za kuutunisha zitakuwa zinapatikana kupitia harambee na wafadhili.
Akiutangaza mfuko huo utakaojulikana kwa jina la ‘Bernard Membe Scholarship, waziri huyo aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya chuo hicho, alisema fedha za kuutunisha zitakuwa zinapatikana kupitia harambee na wafadhili.
Hata hivyo, alisema: “Mfuko huu utakuwa ni wa wazi na fedha zote
zitakazoingia ni lazima zijulikane zimetoka wapi, ili tusije tukaingia
mkenge wa kupata fedha kama za escrow zikatumika kumsomesha mwanafunzi,
mwishowe atajisikiaje?”
Akaunti ya escrow kwa sasa ndiyo ‘habari ya mjini’ na Rais Jakaya
Kikwete anasubiriwa kutekeleza maazimio ya Bunge yanayoeleza jinsi ya
kuwawajibisha baadhi ya mawaziri na watendaji wengine waliohusishwa na
uchotaji wa Sh306 bilioni katika akaunti hiyo iliyokuwa Benki Kuu ya
Tanzania (BoT). Akaunti hiyo ilifunguliwa ili kuhifadhi fedha za malipo
ya gharama za uwekezaji kutokana na mgogoro baina ya Tanesco na IPTL
lakini kabla ya uamuzi wa nani mmiliki halali kutolewa, fedha hizo
zilichotwa i. Kutokana na kitendo hicho, uchunguzi ulifanyika na Bunge
kuazimia baadhi ya vigogo wawajibishwe ama kwa kutoa uamuzi au kupokea
sehemu ya fedha hizo.
Mahafali
Akiwatunuku wahitimu 90 wa shahada ya uzamili, shahada ya kwanza,
diploma na cheti katika mahafali ya pili ya UB katika viwanja vya Hoteli
ya Kiromo, Bagamoyo mwishoni mwa wiki, Membe alisema amebaini kuna
tatizo kubwa la ukosefu wa fedha za kusomesha wanafunzi vyuo vikuu na
wengi wameacha kwa kukosa uwezo, hivyo mfuko wake utawasomesha.
Alisema amefikia uamuzi huo kwa sababu anaamini elimu ni rasilimali na
urithi wa pekee katika maisha ya binadamu hasa katika ulimwengu huu wa
sayansi na teknolojia.
Alisema vijana wanahitaji kupata elimu ya juu lakini familia zao hazina
uwezo wa kulipa ada, hivyo mfuko wake aliouanzisha utawapa nafasi ya
kuwasilisha maombi na wahusika wakiridhishwa na vigezo, watasomeshwa .
Aliwaomba watu wote wenye uwezo, kuchangia mfuko huo ili vijana wote
nchini wanaohitaji elimu lakini hawana uwezo wapate fursa hiyo. Makamu
Mkuu wa chuo hicho, Profesa Costa Mahalu alimshukuru Membe kwa uamuzi
huo na kusema hata bodi ya mikopo nchini haitoshelezi idadi ya wanafunzi
wanaohitaji mikopo kwa ajili ya elimu ya juu.
Kenyatta
Katika tukio jingine, Membe amempongeza Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta
kwa kufutiwa kesi ya uhalifu dhidi ya binadamu iliyokuwa ikimkabili
katika Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai, (ICC) iliyopo The
Hague, Uholanzi. Mwishoni mwa wiki, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC,
Fatou Bensouda aliondoa kesi dhidi ya Kenyatta akisema amekosa
ushirikiano wa Serikali ya Kenya.
Nyongeza na Ibrahim Yamola.Bagamoyo. Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amezindua mfuko wa elimu wa
kusomesha wanafunzi waliofaulu kwenda vyuo vikuu lakini familia zao
hazina uwezo katika Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UB) huku akichukua hadhari
dhidi ya kupokea “fedha kama zile za Akaunti ya Tegeta Escrow”.
Akiutangaza mfuko huo utakaojulikana kwa jina la ‘Bernard Membe
Scholarship, waziri huyo aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili
ya chuo hicho, alisema fedha za kuutunisha zitakuwa zinapatikana kupitia
harambee na wafadhili.
Hata hivyo, alisema: “Mfuko huu utakuwa ni wa wazi na fedha zote
zitakazoingia ni lazima zijulikane zimetoka wapi, ili tusije tukaingia
mkenge wa kupata fedha kama za escrow zikatumika kumsomesha mwanafunzi,
mwishowe atajisikiaje?”
Akaunti ya escrow kwa sasa ndiyo ‘habari ya mjini’ na Rais Jakaya
Kikwete anasubiriwa kutekeleza maazimio ya Bunge yanayoeleza jinsi ya
kuwawajibisha baadhi ya mawaziri na watendaji wengine waliohusishwa na
uchotaji wa Sh306 bilioni katika akaunti hiyo iliyokuwa Benki Kuu ya
Tanzania (BoT). Akaunti hiyo ilifunguliwa ili kuhifadhi fedha za malipo
ya gharama za uwekezaji kutokana na mgogoro baina ya Tanesco na IPTL
lakini kabla ya uamuzi wa nani mmiliki halali kutolewa, fedha hizo
zilichotwa i. Kutokana na kitendo hicho, uchunguzi ulifanyika na Bunge
kuazimia baadhi ya vigogo wawajibishwe ama kwa kutoa uamuzi au kupokea
sehemu ya fedha hizo.
Mahafali
Akiwatunuku wahitimu 90 wa shahada ya uzamili, shahada ya kwanza,
diploma na cheti katika mahafali ya pili ya UB katika viwanja vya Hoteli
ya Kiromo, Bagamoyo mwishoni mwa wiki, Membe alisema amebaini kuna
tatizo kubwa la ukosefu wa fedha za kusomesha wanafunzi vyuo vikuu na
wengi wameacha kwa kukosa uwezo, hivyo mfuko wake utawasomesha.
Alisema amefikia uamuzi huo kwa sababu anaamini elimu ni rasilimali na
urithi wa pekee katika maisha ya binadamu hasa katika ulimwengu huu wa
sayansi na teknolojia.
Alisema vijana wanahitaji kupata elimu ya juu lakini familia zao hazina
uwezo wa kulipa ada, hivyo mfuko wake aliouanzisha utawapa nafasi ya
kuwasilisha maombi na wahusika wakiridhishwa na vigezo, watasomeshwa .
Aliwaomba watu wote wenye uwezo, kuchangia mfuko huo ili vijana wote
nchini wanaohitaji elimu lakini hawana uwezo wapate fursa hiyo. Makamu
Mkuu wa chuo hicho, Profesa Costa Mahalu alimshukuru Membe kwa uamuzi
huo na kusema hata bodi ya mikopo nchini haitoshelezi idadi ya wanafunzi
wanaohitaji mikopo kwa ajili ya elimu ya juu.
Kenyatta
Katika tukio jingine, Membe amempongeza Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta
kwa kufutiwa kesi ya uhalifu dhidi ya binadamu iliyokuwa ikimkabili
katika Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai, (ICC) iliyopo The
Hague, Uholanzi. Mwishoni mwa wiki, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC,
Fatou Bensouda aliondoa kesi dhidi ya Kenyatta akisema amekosa
ushirikiano wa Serikali ya Kenya.
No comments:
Post a Comment