Balozi Seif Ali Idd aweka wazi CCM imejipanga kudhibiti wenye nia ya kuvuruga uchaguzi mkuu ujao
Mlezi
wa CCM Mkoa wa Magharibi Balozi Seif akimkabidhi kadi mwanachama
Thuwaiba Jeni Pandu akiwa miongoni mwa wanachama wapya wa CCM na Jumuia
zake kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Tawi la CCM Pangawe
Jimbo la Fuoni.
Na Othman Khamis Ame.
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Mlezi
wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Magharibi ambae pia ni Mjumbe wa Kamati
Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif Ali Iddi,
amewahakikishia wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwamba uchaguzi Mkuu
ujao wa mwaka 2015 unatarajiwa kuwa wa utulivu na amani.
Amesema
serikali kupitia vyombo vyake vya dola itahakikisha kuwa vikundi vya
kihuni vinavyoanza kuandaliwa kwa ajili ya kuvuruga uchaguzi huo
vinathibitiwa kwa nguvu zote.
Balozi
Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameeleza hayo
wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa
Kwamabata Magogoni, baada ya kumaliza ziara ya siku mbili ndani ya Mkoa
wa Magharibi akiwa mlezi wa CCM Mkoa wa huo.
Amewaomba
wafuasi wa vyama vya upinzani hapa Nchini kuamua mapema kufuata chama
chenye muelekeo wa kuleta maendeleo ya wananchi, ambacho kwa hivi sasa
ni chama cha Mapinduzi.
Wanachama
wapya 50 wa Chama cha Mapinduzi na Jumuia zake wa Jimbo Jimbo la Fuoni
wakila kiapo cha utii baada ya kukabidhiwa kadi kwenye mkutano wa
hadhara hapo Tawi la CCM Pangawe.
Amefahamisha
kwamba ushindi wa chama cha mapinduzi mwaka 2015 hauna mbadala kutokana
na ilivyojipanga na kuungwa mkono na wananchi walio wengi hapa Nchini.
Balozi
Seif Ali Iddi amewatahadharisha wana CCM na wananchi wote kujiepusha
na wimbi la vikundi vilivyokubali kujiingiza katika vitendo vya ugaidi
ambayo kamwe havikubaliki kitaifa wala kimataifa.
Amesema
serikali zote mbili kupitia vyombo vyote vya dola zitakuwa makini
kufuatilia mienendo ya watu hao na kuwashughulikia kwa mujibu wa sheria
zilizopo.
Vijana
wa matambuizo wa Umoja wa Vijana wa CCM Jimbo la Mtoni wakifanya vitu
vyao wakati wa mkutano wao na Mlezi wa Mkoa wa Magharibi Balozi Seif
aliyefanya ziara kukagua maendeleo ya Chama Mkoani humo.
Katika
Mkutano huo wa hadhara Balozi Seif ambae pia ni Naibu Kamanda wa Taifa
wa Umoja wa Vijana wa CCM Tanzania amewatawadha makamanda wa Vijana wa
Majimbo na Wilaya zilizomo Mkoa wa Magharibi Kichama baada ya kuteuliwa
na Baraza Kuu la UVCCM.
Makamanda
hao ni Mh. Thuwaiba Kisasi Kamanda wa Mkoa wa Magharibi, Kanal mstaafu
Masoud Khamis Wilaya, Ibrahim Ramadhan Jimbo la Mtoni, Fatma Adam Jimbo
la Bububu, Bimkubwa Nassor Jimbo la Mfenesini, Ibrahim Raza Jimbo la
Dimani, Hafidh Tahir Ali Jimbo la Fuoni, Ahmada Abdullwakil Jimbo la
Mwanakwerekwe na Abass Hassan Juma Jimbo la Magogoni.
Mlezi
wa CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akikagua Jengo
la Kituo cha Afya cha Jimbo la Mtoni ambalo lililoanzishwa kwa mchango
wa Wananchi na Viongozi waliopita wa jimbo hilo.(Picha na Hassan Issa wa
– OMPR – ZNZ).
No comments:
Post a Comment