Sunday, November 30, 2014

CHONDE CHONDE ULEVI NOMAA, MJESHI AZIMA KWA POMBE


Wananchi  Iringa  wakimtazama  askari wa  jeshi  ambae  jina halikuweza  kufahamika aliyekuwa  amezima kwa ulevi uliopindukia
mjeshi  huyo akiwa  akiwa  amezima
Mjeshi   huyo  akiwa amepata  fahamu baada ya  kumwagiwa maji
 Mjeshi  akiwa amezima kwa  kunywa  pombe  kupita  kiasi 
..........................................................................................................
KATIKA hali isiyotegemewa askari mmoja wa jeshi la kujenga Taifa (JKT) anayesadikika kuwa na wa kambi ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa usiku wa leo amenusurika kuvuliwa nguo za jeshi hadharani baada ya kukutwa amelewa chakali na kulala katika mfereji wa maji machafu eneo la nje ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa
 Tukio hilo lilitokea muda wa saa 2 usiku baada ya wasamaria wema kumshusha askari huyo kutoka katika basi la Mgumba ambalo alikuwa amepanda kutoka Mafinga kuja mjini Iringa.
 Akisimulia kisa na mkasa wa askari huyo kulewa chakali kiasi cha kushindwa kujitambua mmoja kati ya wasamaria wema aliyejitolea kumshusha katika basi hilo alisema kuwa askari huyo alipanda basi hilo Mafinga huku akiwa amelewa na wakati wote wa safari alionekana akinywa pombe kali kiasi cha kushindwa kujimudu na kuanza kutapika na kujisaidia haja ndogondani ya basi hilo.
 Hata hivyo alisema baada ya kufika stendi ilikuwa ni vigumu kujitambua hivyo kupoteza fahamu na kulazimika kumpa msaada na kumzimua kwa maji kabla ya kupata fahamu kiasi na kujificha chini ya mfereji wa maji machafu . 
 Alisema kuwa mara baada ya kujitambua kiasi aliweza kutoa namba ya ndugu yake ambae ni askari wa FFU mjini Iringa aliyefika kumnusuru kuvuliwa nguo na kiongozi wake aliyefika eneo hilo na kumkutana akilishushia heshima jeshi kwa ulevi uliopitiliza
" Umelidhalilisha sana jeshi kwa askari kulewa hivi ukiwa katika sare .....sasa nataka kukuvua sare kisha nakupeleka kulala polisi kabla ya kesho kukuchukulia hatua zaidi " alisikika akisema kiongozi huyo ambae jina wala cheo chake hakukitaja
 Maamuzi hayo ya kiongozi wake yaliwafanya mashuhuda kumuangukia na kumwomba amsamehe kwani bado ni kijana mdogo sana mambi ambayo aliyakubali na ndugu zake kumpakiza katika Taxi na kumpeleka eneo la Kihesa .
 Ushauri wetu kwa askari wetu kujaribu kuheshimu nafasi hizo japo hakuna anayewakataza kunywa pombe ila watambue kuwa unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako ama chonde chonde ulevi nomaaa

HUU NI UNYAMA WA KUTISHA IRINGA ,KIJANA ACHOMWA KISU UTUMBO WATOKA NJE ,

mpenzi mdau wa mtandao huu kwanza naomba radhi kwa picha hizi za kusikitisha ila ndio hali halisi ya mambo inatisha sana Kijana kizito Kimeya (28) mkazi wa kijiji cha Mkoga kata ya Isakalilo Manispaa ya Iringa akiwa Hospitali ya mkoa wa Iringa kupatiwa matibabu baada ya kuchomwa kisu na utumbo wake kutoka nje
Miguu ikiwa imekatwa katwa mapanga na wauwaji hao ambao hawakufanikiwa kutimiza azmayao
hapa utombo ukiwa nje baada ya kuokolewa na afisa mtendaji wa kata hiyo ya Isakalilo Iringa mjini
Ni vigumu kuamini kama kweli kuna binadamu na wanywa damu ila kutokana na matukio kama hayo ndipo unaweza kuamini kuwa wapo binadamu na wanywa damu baada ya watu wanne ambao majina yao yametajwa na kijana huyo kudaiwa kumchoma visu kijana huyo pichani baada ya kumfuma akiiba mahindi ya mabichi maarufu kama Gobo katika shamba lao Kijana huyo alichomwa kisu na kucharangwa mapanga na baada ya wahusika kutenda unyama huo walimchukua na kumweka katika mfuko wa sarufeti na kujaza mchanga na kisha kumtupa mtoni kabla ya na kusindwa katika maji kwa masaa zaidi ya matano na baadae maji kusaidia kuupasua mfuko huo na mchanga wote kumwagika na kijana huyo kujisaidia kujikokota hadi nje kavu na kukutwa porini siku ya pili yake majira ya saa 1 usiku na wasamaria wema.

RAIS Kikwete awasili nchini



 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mmoja wa abiria wakati ndege aliyopanda ilipotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu wa Rais Bw. Morris Mbena baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea

Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam baada ya kuwasili akitokea Marekani kwenye matibabu leo

Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia mkono wafanyakazi  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam baada ya kuwasili akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba

29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Majeshi Jenerali davis Mwamunyange baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP  Ernest Mangu baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza John Minja  baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama Bw. Rashid Othman baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mama Maria Nyerere baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikumbatiana kwa furaha  na Mama Maria Nyerere baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru  Mama Maria Nyerere baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Mama Maria Nyerere akiongea na Mama Salma Kikwete katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam baada ya Rais Kikwete kuwasili akitokea Marekani kwenye matibabu leo

Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiongea na Mama Maria Nyerere aliyefika kuwapokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na waandishi wa habari na viongozi mbalimbali waliokuja kumlaki baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na waandishi wa habari na viongozi mbalimbali waliokuja kumlaki baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
Dua ilisomwa na viongozi mbalimbali wa dini  baada ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete kumaliza kuongea na wanahabari mara tu alipowasili  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Marekani kwenye matibabu leo Novemba 29, 2014
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia wafanyakazi wa ikulu waliojitokeza kumpokea mara baada ya kuwasili ikulu akitokea nchini Marekani kwenye matibabu
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia kwa furaha wafanyakazi wa ikulu waliojitokeza kumpokea mara baada ya kuwasili ikulu akitokea nchini Marekani kwenye matibabu
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea mashada ya maua kutoka kwa wafanyakazi wa Ikulu waliojitokeza kumpokea mara baada ya kuwasili Ikulu akitokea nchini Marekani kwenye matibabu. Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue aliyeongoza mapokezi hayo ya Ikulu 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea kadi ya pole toka kwa mjukuu wake Aziza Ridhiwani Kikwete mara baada ya kuwasili Ikulu 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa kwa furaha na mwanaye Khalfani baada

KENYA – KAMPENI ZA KUKUMBUSHIA UADUI WA KIFAMILIA

Raila Odinga vs Uhuru Kenyatta 

Mwanzoni mwa miaka 1980 Jaramogi Oginga Odinga alikuwa katika wakati mzuri kujifufua kisiasa na akatumia nafasi ya kisiasa kumsimanga rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta kama mkwapuaji wa ardhi. Leo hii Raila Odinga, mtoto wake anayegombea urais wa Kenya kwa Muungano wa Mageuzi na Demokrasia - CORD naye anatumia kibwagizo cha baba yake kwa kusema kuwa Uhuru Kenyatta, mgombea wa Muungano wa Jubilee ni mkwapuaji ardhi. 

Ukitizama historia ya Kenya, baada ya kifo cha rais Jomo Kenyatta na Rais Daniel Arap Moi kuchukua nafasi yake mwaka 1978, alijaribu kuhakikisha wapigania uhuru wote ambao walihitilafiana na hayati rais Kenyatta anawarudisha serikalini na kuwapa vyeo katika kujaribu kujenga umoja wa kitaifa. Oginga Odinga aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya Pamba ambayo ilimuwezesha kurudia harakati zake za kisiasa. Siku moja alihutubia mkutano wa hadhara aliamua aeleze ni kwanini alikosana na Hayati Kenyatta na akasema sababu kubwa ilikuwa eti rais Kenyatta alikuwa rais aliyekuwa anatetea wachache matajiri wakati yeye alikuwa anaamini katika falsafa ya fursa sawa katika kumiliki ardhi na kuwapa upendeleo maalum kwa masikini wanaohitaji ardhi. Baada ya Oginga Odinga kuueleza umma ni kwanini alikosana na hayati Kenyatta, rais Daniel Arap Moi alichukizwa na kauli zake na mara moja aliagizwa akamatwe tena na akawekwa kizuizini hadi miaka ya 1990 wakati harakati za demokrasia ya vyama vingi ziliposhika kasi. 

Kinachotokea kwa sasa nchini Kenya ni marudio ya enzi ambapo watoto wa Kenyatta na Oginga Odinga wanachuana katika kupata madaraka katika uchaguzi wa mwezi ujao. Suala la ardhi limejitokeza kuteka vichwa vya habari hasa pale Raila Odinga wakati akizindua kampeni zake za kisiasa alikumbushia kuwa familia ya Uhuru Kenyatta inamiliki ardhi kubwa ya ukubwa wa eneo zima la Jimbo la Nyanza. Katika kujaribu kujisafisha, Uhuru Kenyatta aliwambia watu katika kampeni zake kuwa kama kuna mtu ana ushahidi wa ukwapuaji wa ardhi uliofanywa nay eye akamshtaki mahakamani. Na akaongezea kuwa yeye si mkwapuaji ardhi ila Raila Odinga lazima ajibu tuhuma za kukwapua kiwanda cha molasses (sukari guru) huko Kisumu.

 WELEDI WA WAGOMBEA WA KISIASA 

Kimsingi, Raila Odinga ameamua kutumia suala la ardhi kama eneo lenye udhaifu kwa weledi wa Uhuru Kenyatta. Nikumbushe kuwa hakuna mtu amewahi kupima na kujua ukubwa wa ardhi inayomilikwa na familia ya Kenyatta. Lakini inachukuliwa kama ni ukweli usiopingika kuwa ardhi ya familia ya Kenyatta inasemekana inaanzia Pwani ya Kenya hadi kukutana na Jimbo la Bonde la Ufa. Uhuru wa Kenyatta anabakia kuwa kama mtu anayeishi kwa kufaidi matunda yaliyokwapuliwa na baba yake; lakini tujiulize je ni sahihi kwa mtoto kulipa dhambi zilizofanywa na baba yake? Kama watanzani ni vyema tujifunze kitu kutokana na yanayotokea nchini Kenya kwa sasa. Ardhi ni jambo la kuangaliwa kwa umakini sana duniani kote. Ninaiona hizi kukashifiana kati ya Kenyatta na Odinga kama kukosa busara na ni aina ya ubaguzi wa kisiasa uliojaa unafiki wa hali ya juu (disingenuous). 

Ukifuatilia siasa za Kenya ni nchi ambayo ilichagua kufuata sera za kibepari ambazo zinazingatia umiliki binafsi wa mali (private ownership) na wala si umilikaji mali kwa pamoja (collectivism). Ubepari ni mfumo uliojaa kutokujali haki, usawa,na kushadidia utendaji wa kutokujali taratibu. Kwa kuzingatia sera za kibepari, ardhi ikishanyakuliwa hairudi tena. Ukisoma historia, kwa mfano, wakati wavamizi kutoka uingereza waliponyakua ardhi za wenyeji wa Amerika kule Manhattan ndio ilipotea kabisa na walionyakuwa wakaiendeleza. Raila Odinga anachofanya ni kujaribu kupata umaarufu wa kisiasa (cheap politics) na wote wawili ni kielelezo cha siasa za hovyo za kiafrika. Raila Odinga anachotukumbusha ni kuwa sasa ni wakati kwa Uhuru Kenyatta kuona ukwapuaji wa ardhi uliofanywa na baba yake anaurekebisha kwa kuwarudishia ardhi hiyo wale ambao hawana ardhi na walifukuzwa maeneo hayo wakati huo wa ukoloni.

 Ni jukumu la wanasiasa wa leo kutuonesha kuwa dhambi za tawala za zamani zifutwe na zisiendelezwe tena kipindi cha sasa. Yaani anamaanisha eti Uhuru Kenyatta anapaswa kutumia kampeni hizi kuwaahidi wakenya ambao walifukuzwa kwenye ardhi zao na kunyakuliwa na baba yake Mzee Kenyatta kuwa atawarudishia kiasi fulani cha ardhi ambayo baba yake alitumia madaraka vibaya kwa kuamua kujimegea ardhi kutoka kwa wakoloni wa kiingereza na kutowarudishia walionyang’anywa yaani Wakenya wenzake. 

WANASIASA NI WAONGO 

Kimsingi, Uhuru Kenyatta alikuwa na umri mdogo sana wa miaka 15 wakati Mzee Kenyatta anafariki dunia. Kusema yeye ndiye aliyerithi ardhi ya baba yake ni makosa; ila ardhi hiyo ilirithiwa na mama yake (Mama Ngina) na ndugu wa familia nzima. Kama kweli Uhuru Kenyatta ataamua kuwarudishia ardhi wasio na ardhi nadhani itakuwa kama kuwahonga wapiga kura kwa sasa. Isipokuwa Uhuru Kenyatta kukataa kuwa yeye si mfaidika wa ukwapuaji ardhi Kenya inatufikisha mahali tuwe makini na wanasiasa wetu wa kiafrika. Ni waongo sana na si watu wa kukubali ukweli na kuukabili kama ulivyo. Kwa upande wa Raila Odinga, yeye amekazia kumshambulia Uhuru Kenyatta na anawaahidi wakenya wakimchagua atahakikisha wenye ardhi kubwa wanazirudisha. Sina hakika kama yuko sahihi, ikumbukwe kuwa Kenya sasa inatawaliwa na Katiba mpya kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita sasa; na ukiisoma Katiba ya Kenya ndicho chombo pekee ambacho kimeweka utaratibu wa kuhakikisha wale walionyang’anywa ardhi wanarudishiwa. Hakuna mwanasiasa yeyote atakayeweza kurudisha au kunyang’anya mtu ardhi.

 Kama Raila Odinga anataka kuwa mkweli, ni bora aeleze ni jinsi gani atasimamia kuhakikisha Sera ya ardhi, Sheria ya Ardhi na Katiba ambayo imeweka kipengele (Sura nzima) maalum kueleza ni jinsi gani watu waliopoteza ardhi watarudishiwa au kulipwa fidia ya ardhi yao. Sera ya ardhi ya Kenya imeelezea kinagaubaga juu ya historia ya tatizo la ardhi nchini Kenya na ikaweka njia mbadala kutatua tatizo hili. Hii imejenga msingi kwa Katiba mpya ya Kenya kutekeleza sera ya ardhi. Kwa ujumla, kampeni hii ya kufufua chuki za wazazi wa wagombea ni kielelezo kingine kuonesha kuwa kwa kiasi fulani wanasiasa wetu ni wabinafsi zaidi na kwenye kampeni hawazungumzi mambo ya msingi (issues) bali wanabakia wakizungumza siasa katika kutafuta mvuto wa kisiasa zaidi (political mileage). Tunapojiandaa kwa mabadiliko ya kisiasa Tanzania tunapaswa kuyachambua kwa kina matamko ya wanasiasa wetu.

PICHA ZA LULU AKIWA KATIKA KABURI LA KANUMBA

 Jana ilikua ni siku ya kumbukumbu ya kifo ch amarehem Kanumba, ambae alikua anafikisha mwaka mmoja tangu alipofariki, mastar wa movie wengi walikuwepo katika kuhakikisha shughuli hiyo inaenda vizuri, ikiwa ni pamoja na kutembelea kaburi la Kanumba.

Lulu akilia juu ya kaburi la Kanumba 

Lulu na mama yake Kanumba

Irene Uwoya

Lulu katika kaburi la Kanumba

ALEX FERGUSON AFANYA INTERVIEW KALI

Kocha Alex Ferguson wa Man U amefanya mahojiano na gazeti moja huko Uingereza (Football Focus) na kuzungumzia mambo mengi kuhusu ufundishaji na menejiment ya timu ya mpira wa miguu hasa wakati wake akiwa na Klabu ya Man U. Amezungumzia mambo kadhaa ya msingi katika maeneo yafuatayo: 1. KUHUSU MAN CITY: Anasema ni timu hatari na wapinzani wao haswa kwa sasa kama ilivyokuwa zamani ilivyokuwa Chelsea. 2. KUHUSU RVP: Sir Alex anasema hakuwahi kudhani siku moja angeliweza kumsajili Robin Van Persie. Anasema alizungumza muda mrefu na Wenger na majadiliano yao yalikuwa mazuri ingawa hakudhani Arsenal wangekubali kumuuzia mchezaji huyo. Ila aligundua baadaye Arsenal waligundua RVP anataka kuhama na hivyo ikawa rahisi kumpata. 3.UCHEZAJI WA RVP: Ni mchezaji mwenye ujuzi wa mchezo na uwezo wake umetoa faraja kwa watu wote hapa Man U. 4. UMUHIMU WA KUHUDHURIA MAZOEZI: Sir Alex anasema hajawahi kuacha kuhudhuria vipindi vya mazoezi hata siku moja. Uangalizi wake ni muhimu sana katika kipindi hiki cha maisha yake. 5. SUALA LA UFUASI KATIKA MCHEZO WA MPIRA:Sir Alex anasema hivi: "Wapo watu miongoni mwa wasaidizi/wafanyakazi wangu ambao wamekuwa na mimi kwa miaka 20 au zaidi. Hii inaleta hali ya ufuasi kwangu na mimi kwao pia". 6.KISASILI/MYTHIOLOGIA ZAKE: Sir Alex anazungumziaje kuhusu visasili juu ya maisha yake? "Visasili ni vingi sana juu ya maisha ya watu waliofanikiwa. Mojawapo ya uzushi mkubwa juu ya maisha yangu ni eti nimewahi kufanya kazi kwenye bandari. Anasema hajawahi kufanya kazi bandarini kamwe, ila baba yake, kaka zake na wajomba zake walifanya kazi bandarini.Sir Alex anadai kuwa alikuwa mwerevu zaidi (intelligent) kutokufanya kazi za bandari. 7. JOSE MOURINHO: Sir Alex anadai huyu ni mtu anayependa kucheza na mchezo wa kupandisha presha "mind game" dhidi ya timu pinzani. Huwezi kujua atafanya nini huwa hashindani naye kwani huwezi kumshinda. Anasema "huwa sishindani naye na huwa ananiletea chupa ya wine kila mara. 8. REAL MADRID: Nawaangali Real Madrid kila weekend usiku; aliwaangalia wakicheza na Granada na anaamini Ronaldo alifunga goli zuri sana ila tu ilikuwa ni siku ya Granada. Kuhusu mchezo wa Champions ligi dhidi ya Madrid (13/2/2013) anasema anawajua uimara wao na ni lazima apange kikosi sahihi siku hiyo ili washinde. Utakuwa mchezo mgumu sana na hawa jamaa hawafungiki kirahisi Bernabeu. 9. WACHEZAJI KUWA MAKOCHA: Sir Alex anasema: "Tunaona hali ambapo mtu anakuwa mchezaji leo alafu baadaye kocha.Hebu niambieni hii inawezekanaje? Ninajisomea sana kuhusu kuwaharakisha wachezaji kuwa mameneja eti kwasababu tu wamewahi kuwa wachezaji wa kimataifa.Haijalishi mtu umekuwa mchezaji wa kimataifa au hujawahi kucheza ligi yoyote, ili kuwa na mafanikio katika kazi ya umeneja wa timu ni lazima uwe na kipindi kirefu cha kujifunza chini ya uangalizi wa meneja mzoefu. 10.KUSTAAFU KAZI YA UMENEJA: "Hili swali linajirudia mara nyingi kadri ninavyoendelea kuzeeka.Nadhani jambo la msingi ni kwa vipi ninajisikia. Kadri mtu unavyozeeka hali afya haitabiriki hasa katika umri wa miaka 70 na kuendelea. Hadi sasa hivi hali yangu ya afya ni murua; ila huwezi kujua".

UPDF CHINI YA MTOTO WA MUSEVENI UGANDA


Raisi Yoweri Kaguta Museveni ni kiongozi ambaye amefanikiwa kuirejesha Uganda katika ramani ya dunia kutoka katika hali isiyokuwa ya utulivu hadi katika maendeleo. Wakati anakaribia kustaafu; ameamua kulifanya Jeshi la nchi hiyo kuwa chini ya mtoto wake Muhoozi Kainerugaba.
Raisi Museveni tayari amepinga imani ya baadhi ya wapinzani wake juu ya hiki kinachoonekana ni kumuandaa mtoto wake Muhoozi kama ndiye mtu mwenye nguvu kuliko Mkuu wa Majeshi.

UHURU KENYATTA ASHINDA URAIS KENYA




Uhuru Muigai Kenyatta ameshinda urais wa Kenya kupitia muungano wa Jubilee kati ya chama chake cha TNA na URP cha Willium Ruto ambaye atakuwa makamu wa Raisi.  Ni uchaguzi ambao umeendeshwa kwa umakini mkubwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) ingawa imechukuwa siku nyingi kwa matokeo kutangazwa. Kimsingi ni uchaguzi ambao utakuwa umeuwa ndoto ya kisiasa ya Raila Odinga kuwa Raisi wa Kenya maisha yake yote.

FIFA YATOA ORODHA YA WACHEZAJI 23 WANAOWANIA BALLON D’OR 2014.


Shirikisho la soka duniani FIFA limetangaza majina ya wachezaji 23 wanaowania tuzo ya FIFA ya Ballon d’Or mwaka 2014.

Wachezaji sita wa Ujerumani waliocheza Kombe la dunia wametajwa, na kufanya iwe nchi yenye wawakilishi wengi kwenye orodha hiyo. Wachezaji hao wa Ujerumani ni Philipp Lahm, Mario Gotze, Toni Kroos, Thomas Muller, Manuel Neuer na Bastian Schweinsteiger.
Cristiano Ronaldo anayeshikilia tuzo hiyo na mshindi mara nne Lionel Messi wapo tena katika mchakato huo
ORODHA YA WACHEZAJI 23 WANAOWANIA BALLON d’Or
Gareth Bale (Wales), Karim Benzema (France), Diego Costa (Spain), Thibaut Courtois (Belgium), Cristiano Ronaldo (Portugal), Angel Di Maria (Argentina), Mario Gotze (Germany), Eden Hazard (Belgium), Zlatan Ibrahimovic (Sweden), Andres Iniesta (Spain), Toni Kroos (Germany), Philipp Lahm (Germany), Javier Mascherano (Argentina), Lionel Messi (Argentina), Thomas Muller (Germany), Manuel Neuer (Germany), Neymar (Brazil), Paul Pogba (France), Sergio Ramos (Spain), Arjen Robben (Holland, James Rodriguez (Colombia), Bastian Schweinsteiger (Germany), Yaya Toure (Ivory Coast).


 
Umri: 28 Thamani ya utajiri wake: $13.8 billion WASIFU WAKE: Aliwahi kuishi chumba kimoja na Mark Zuckerberg, Alikuwa moja ya wafanyakazi kampuni ya Facebook ambayo ana mchango mkubwa katika kuanzishwa kwake, Hadi sasa Moskovitz huwa anatumia usafiri wa baisikeli kwenda kazini. Anapanda ndege za wananchi wa kawaida anaposafiri.
Namba 2 ni Mark Zuckerberg
Mark Zuckerberg
Umri: 28
Thamani ya utajiri wake: $13.3 billion
WASIFU WAKE: Ndio mwanzilishi wa Mtandao wa kijamii maarufu wa Facebook ambao ndio chanzo kikuu cha utajiri wake.


Namba 3 ni Albert von Thurn und Taxis
Albert von Thurn und Taxis
Umri: 29
Thamani ya utajiri wake: $1.5 billion
WASIFU WAKE: Jina lake liliingia katika orodha ya Matajiri inayoandaliwa na Forbes akiwa na umri wa miaka 8, lakini alirithi rasmi utajiri aliokuwa nao mwaka 2001 alipotimiza miaka 18, Ni mpenzi mkubwa wa Rally za magari, Yeye pia hushiriki mbio mbalimbali za magari huko Ujerumani.


Namba 4 ni Scott Duncan
Scott Duncan
Umri: 30
Thamani ya utajiri wake: $5.1 billion
Duncan ni mtoto wa mwisho wa Dan Duncan - Billionea aliyepata utajiri mkubwa kutokana na biashara ya gesi kupitia kampuni ya Enterprise Products Partners ambayo mpaka sasa inamiliki eneo lenye ukubwa wa maili 50,000 zenye gesi asilia na mafuta.

Namba 5: Eduardo Saverin
Eduardo Saverin
Age: 30
Thamani ya utajiri wake: $2.2 billion
Ni moja ya waanzilishi wa Facebook pia, Alijivua uraia wa Marekani mwaka 2011, na alishawahi kuingia katika vita kali ya maslahi na Facebook na kutulia baada ya kupewa asilimia 5 za shares, Kwa sasa anaishi huko Singapore ambapo anaendesha biashara zake nyingine.