Tuesday, March 24, 2015

Watu 6 Wafariki Dunia Usiku Wa Kuamkia Leo baada ya Magari Manne Kugongana Huko Nzega.....Hapa kuna Picha 10 Toka Eneo la Ajali


Watu 6 wamefariki  dunia  na  wengine  9 kujeruhiwa  vibaya  katika  ajali  mbaya   iliyohusisha  magari  manne  huko Undomo wilayani Nzega  usiku  wa  kuamika  leo.








Sunday, March 22, 2015

Maamuzi ya Mahakama kuhusu kesi inayomkabili Chris Brown!!


brown

Baada ya kutumikia kifungo cha miaka sita akihukumiwa kwa kosa la kumpiga aliyekuwa girlfriend wake Rihanna, kuna maamuzi ambayo mahakama ya Los Angeles imetoa kuhusiana na hitmaker wa nyimbo ya ‘New flameChris Brown.
Ni miaka sita tangu mwanamuzi Rihanna amshtaki Chris Brown kwa kosa la kumpiga na kutumikia adhabu hiyo ambayo alikuwa katika kipindi cha majaribio na sasa yuko huru baada ya kesi yake kumalizika.
Katika kuonyesha furaha yake Chris Brown baada ya kutoka mahakamani hapo aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa anamshukuru  Mungu kwa kuwa yupo huru.
“IM OFF PROBATION!!!!!!!! Thank the Lord!!!!!!”

Zitto ajiunga rasmi na Chama cha ACT-Tanzania, akabidhiwa kadi namba 007194

_MG_7774
Mh. Zitto Kabwe akilipa kwa ajili ya usajili wa kadi ya uanachama wa ACT.
...Kumwaga ‘mboga’ mbele ya wandishi wa Habari Jumapili hii Machi 22
Na Andrew Chale wa Modewji blog
Hayawi hayawi…Sasa yamekuwa licha ya kusemwa sana kwa muda mrefu juu ya kuhusishwa na chama kipya cha siasa cha ACT-Tanzania dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Ruyagwa Kabwe sasa yamekuwa kweli kwa Mbunge huyo baada ya leo Jumamosi ya Machi 21, kupokelewa rasmi na chama hicho na kukabidhiwa kadi yake yenye namba 007194.
Hii  inafuatia siku moja baada ya Zitto kutangaza kuachia ubunge na kuandika barua rasmi ambapo sasa amekuwa mwanachama wa ACT-Tanzania na kuahidi kuendeleza mapambano ndani ya chama hicho.
_MG_7798
Mh. Zitto Kabwe akisaini kadi ya uanachama wa ACT.
Hata hivyo, kwa mujibu wa viongozi waandamizi wa ACT-Tanzania wamedokeza kuwa, Zitto ataongea na vyombo vya habari Jumapili ya Machi 22.
Endelea kufuatilia EDDY BLOG kwa tukio hilo tutakalowaletea kila kitakachojiri katika mkutano huo, kujua ni wapi na muda gani  endelea kuperuzi nasi.
ACT-Tanzania: kirefu chake ni :  Chama cha Alliance for Change and Transparence (ACT-Tanzania). Makao makuu ya chama hicho yapo Kijitonyama Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
_MG_7819
Mh. Zitto Kabwe akikabidhiwa rasmi kadi ya uanachama wa ACT.
_MG_7825
Mwanachama rasmi wa ACT Mh. Zitto Kabwe akipokea kadi hiyo.
_MG_7829
“He..he he mnipokeee sasa kwa mikono miwili….:, Mh. Zitto Kabwe akionyesha kadi hiyo kwa baadhi ya wanachama waliosimama (hawapo pichani) nje ya ofisi za chama cha ACT tawi la Tegeta,
_MG_7858
Mh. Zitto Kabwe akibadilishana mawazo na viongozi wa Chama cha ACT mara baada ya kupokea kadi hiyo.
_MG_7864
Mh. Zitto Kabwe akiwa amefuatana na Prof. Kitila Mkumbo ambaye pia ni mwanachama wa ACT.
_MG_7893
Mh. Zitto Kabwe akivalishwa skafu ya ACT mara baada ya kupokea rasmi kadi ya chama hicho mapema JANA.
_MG_7958
Na hii ndio kadi rasmi ya Mheshimiwa Zitto Kabwe aliyokabidhiwa.

Saturday, March 21, 2015

NEWS ALERT: NYUMBA ILIYOPO NDANI YA MSIKITI SOWETO YATEKETEA YOTE KWA MOTO MAPEMA LEO.




Jengo lililopo ndani ya Msikiti wa Soweto Limeteketea kwa moto Mapema leo chanzo hakijafahamika bado Moto huo umeteketeza nyumba yote, japo kuwa wananchi na waumini walijitahidi kuzima lakini ulionekana ni mkubwa sana, Hata hivyo wananchi wamelaumu Kikosi cha zimamoto kwa kuwa walipewa taarifa mapema lakini hawakuweza kufika kwa muda katika eneo hilo. Endelea kufuatilia tukio hili hapa kwa taarifa zaidi.

No comments:

Post a Comment