Thursday, March 26, 2015

Aliota ndoto mpenzi wake kampiga kibao usingizini, hiki ndicho alichokiamua na yeye !!

Mwanamke mmoja nchini Nigeria anashikiliwa na Polisi kutokana na kosa la mauaji ya mtu ambaye alikuwa ni mpenzi wake.. kisa chote kilianzia kwenye ndoto !!
bloody_handsMwanamke huyo Monsurat Yusuf alishtuka toka usingizini na kumsimulia mpenzi wake, Eric Moses kwamba ameota ndoto ambayo alihisi amepigwa na mpenzi wake huyo makofi akiwa usingizini.
Eric alicheka baada ya kusikia story hiyo lakini kumbe Monsurat hakupenda, akachukua kisu na kumchoma mpenzi wake huyo ambaye alifariki.
Upelelezi wa Polisi umeonesha wote wawili walikuwa ni wanafunzi na walikuwa wakiimba kwaya pia ya kanisa.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia Twitter,  na Facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza>>>twitter Facebook

No comments:

Post a Comment