Alichokisema mkandarasi na mkubwa Fella kuhusu kuanguka ukuta wa nyumba ya Diamond#U Heard
Kutokana
na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini na kuleta madhara
mbalimbali kuna taarifa kuwa nyumba ya kifahari ya msanii Diamond Platnumz ambayo ujenzi wake haujakamilika imekubwa na madhara ya mvua baada ya ukuta wake kuanguka.

Soudy Brown alimtafuta Diamond bila mafanikio na kuamua kumtafuta meneja wake Said Fella,
ambae amesema kuwa hataweza kuzungumzia kwasababu nyumba hiyo
kakabidhiwa mkandarasi, ila ni kweli ukuta umeanguka kutokana na mvua
zinazoendelea kunyesha lakini bado iko chini ya mkandarasi na anatakiwa
kukabidhi mwezi wa sita, ingawa Diamond ameshahamia kwenye nyumba hiyo mwezi mmoja uliopita lakini hakupata madhara yoyote kutokana na tukio hilo.
No comments:
Post a Comment