Hatma ya TV za Kenya kuhusu ishu ya kurusha matangazo ya digitali

Vituo
vitatu vya runinga vilivyozimwa majuma matatu yaliyopita vitarejea
hewani leo alhamisi kuanzia saa 12 u nusu saa za Afrika Mashariki .
Vituo hivyo ambavyo vinavyodhaniwa kuwa
na ushawishi mkubwa nchini Kenya zimetangaza kuwa zitarejea hewani
kuanzia saa kumi na mbili jioni saa za Afrika Mashariki, baada ya majuma
matatu gizani.
Vituo hivyo ni Citizen TV, KTN, NTV vimekuwa wakilumbana vikali na serikali kuhusu kuhamia mfumo wa digitali, hadi kwenda mahakamani kutafuta suluhu.
Hata hivyo mahakama iliamua kuwa vituo
hivyo havikuwa na la kufanya ila maagizo ya mamlaka inayosimamia masafa
na mawasiliano nchini Kenya kwani walikuwa na muda wa kutosha kuweka
mikakati inayohitajika kuhamisha matangazo yao kutoka masafa ya analojia
hadi yale ya kisasa ya dijitali.
Stesheni hizo ziliomba muda zaidi
kuagiza visanduku vya kunga’mua masafa ya digitali kwa wateja wao huku
wakilalamika kuwa kampuni zilizopewa leseni kusambaza masafa yao
yalikuwa yakitoza ada ya mwezi ilhali hawakuwa wakilipia huduma na
matangazo kutoka kwa stesheni hizo.
No comments:
Post a Comment