Mtoto alikuwa analia, baba yake akaamua kumng’ata ili anyamaze!
Matukio ya unyanyasaji kwa watoto wadogo yameendelea kujitokeza kila kukicha, mwanaume mmoja Felipe Deaquino anashikiliwa na Polisi Stamford, Uingereza kwa kosa la kumg’ata usoni mtoto wake mchanga aliyekuwa akilia.
Polisi walifika nyumbani kwa kijana huyo
baada ya kupata taarifa za mtoto huyo kunyanyaswa na kumkuta mke wake
ambaye aliwaambia Polisi kwamba ana mgogoro na mume wake baada ya kukuta
mate usoni kwa mtoto huyo ambaye ana umri wa miezi sita mchanga mwenye
umri wa miezi 6.
Mwanamke huyo na mtoto wake walipelekwa
Hospitali baada ya kugundua mtoto huyo alikuwa na majeraha makubwa usoni
upande wa kushoto na alikuwa na alama ya kuchomwa moto kwenye kiganja
cha mkono ambapo inasemekana kuwa ilisababishwa na sigara.
Deaquino ambaye umri wake ni miaka 18, alikamatwa
na Polisi na kuhojiwa akakiri kumng’ata mtoto wake mchanga huku akisema
alifanya hivyo kutokana na mtoto huyo kulia, ameshtakiwa kwa makosa
mawili ya kushambulia na baadaye akaachiliwa kwa dhamana ya dola 35,000.
No comments:
Post a Comment