Tuesday, February 24, 2015

Mez B afariki dunia asubuhi ya leo, dada na kaka yake wathibitisha

Msanii wa Bongo fleva aliekuwa anaunda kundi la Chemba Squard, Moses a.k.a Mez B amefariki dunia asubuhi ya leo akiwa nyumbani kwao Dodoma baada ya kuugua kwa muda.
kutokana na kauli ya dada yake mzazi na mdogo wake wa kiume, Mez b ameugua kwa wiki nne mfululizo, alishalazwa takribani mara nne na "kila mara alikuwa akipata nafuu na kurudi nyumbani, lakini leo hii amezidiwa ghafla na ndio akafari." amesema dada wa Mez b.
"Naitwa Recho dada ake na Mez b, amefariki dunia leo asubuhi, kwasasa yupo hospitali, alikuwa anaumwa , alikuwa ana homa na pia alikuwa na tatizo la kuishiwa damu, kwa leo hakuwa amelazwa lakini tulimpeleka baada ya kuwa hali imebadilika, alilazwa wiki iliyopita kwahiyo alipopata nafuu akawa amerudishwa nyumbani, lakini jana alikuwa ok na tukakuta asubuhi alikuwa ok, lakini ilipofika mida ya saa nne hali ikabadilika ndio akafariki, yupo hospitali ya general."

No comments:

Post a Comment