JB KUTOKA NA MZEE WA SWAGA
BAADA ya filamu yake ya Mikono Salama kutesa katika soko la filamu Swahilihood sasa gwiji wa filamu Jacob Stephen ‘JB’ anakuja na filamu kali na ya kusisimua ya Mzee wa Swaga akiwashirikisha wasanii wakali katika tasnia ya filamu ya Bongo.Wasanii walioshiriki katika filamu hiyo ni Wastara Juma ‘Stara’, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’, Wellu Sengo, Cassie Kabwita kutoka nchini Zambia, Nassor Ally, na wasanii wakali kutoka Bongo Movie wameshiriki na kuonyesha uwezo wao.
Mzee wa Swaga inatarajia kutoka wiki hii siku ya Alhamis na kusambazwa katika maduka yoyote ya kuuza filamu Bongo ni kazi iliyotengenezwa katika mikoa ya Dodoma, Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam kuifanya iwe tofauti na sinema nyingine ambazo zinatengenezwa na kampuni za filamu.
No comments:
Post a Comment