Thursday, May 7, 2015

Staa wa filamu za Bollywood kwenye Headlines kwa mara nyingine mahakamani!!

black
Mwaka 2002 mwigizaji filamu maarufu duniani wa Bollywood kutoka India Salman Khan, alishtakiwa kwa kuua bila kukusudia baada ya kuelekeza gari lake kwenye kundi la watu waliokuwa wamelala kando ya barabara huku mmoja wa watu hao akipoteza maisha.
Habari mpya kwa sasa ni kwamba mahakama ya India imemuhukumu kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mtu huyo huku akiwa amelewa mjini Mumbai.
khan
Salman Khan akiwa ndani ya gari huku akizingirwa na waandishi wa habari kabla ya kutolewa hukumu
Khan amedai kuwa dereva wake ndiye anapaswa kulaumiwa kwa tukio hilo lakini mashuhuda wanasema mwigizaji huo ndiye aliyekuwa anaendesha gari na alikimbia baada ya kutokea kwa ajali hiyo.
Baadhi ya filamu ambazo staa huyo aliweza kuigiza na kufanya vyema kwenye soko la filamu duniani ni pamoja na Dabangg, Ready, Bodyguard, Ek Tha Tiger na Maine Pyar Kiya.
Unahitaji chochote ninachokipata kisikupite? jiunge na mimi kwenye TwitterFacebook na Instagram kwa kubonyeza hapa >>> Twitter Insta FB na nitakua nikikutumia kila ninachokipata.

No comments:

Post a Comment