Friday, August 14, 2015

Magufuli Aahidi Ushindi wa Tsunami CCM......Asema Wapinzani Wataishia Kupiga Kelele Tu, Mwigulu Nchemba Naye Apigilia Msumari wa 'Moto'



MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli, amewahakikishia wana-CCM na Watanzaia kwa ujumla kuwa mwaka huu, chama kitapata ushindi wa Tsunami na si wa kishindo wala kimbunga.

Dk Magufuli alisema hayo nje ya ofisi ya chama hicho mkoani Mtwara juzi alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama hicho ambapo alisisitiza kuwa wapinzani watapiga kelele sana, wataongea sana lakini ushindi kwa CCM ni lazima na upo pale pale.

Alisema ushindi huo unatokana na matawi yaliyoanguka ndani ya chama na kuhama na kwamba watu hao wameiacha CCM ikiwa safi na salama zaidi. 
 
Alisema watu hao walikuwa wakitumia fedha nyingi kurubuni watu wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM ambapo chama kiliwakata na kukimbilia vyama vingine vya upinzani.

Aliwataka wana-CCM wasikatishwe tamaa na watu wa aina hiyo na badala yake washikamane, wawe kitu kimoja na kwamba mwaka huu, chama kitafanya kampeni za kisayansi. 
 
Aidha, Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba alisema ni kazi rahisi kumnadi Dk Magufuli kutokana na vigezo na sifa alizonazo.

Mwigulu, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, alisema walioshindwa kwenye mchakato wa kura za maoni na kuhama ndani ya chama, hivi sasa wanahaha kutafuta urais wenyewe ambapo wanatoa mpaka hela ili kutafuta uongozi, lakini wataumbuka mapema.

Akizungumza na mamia ya wana-CCM waliojitokeza kumpokea katika hiyo ofisi ya chama ambapo alifika kwa ajili ya kuwasalimia na kuwashukuru kwa kumchagua kuwa mgombea na kumdhamini, Dk Magufuli aliwataka makada hao na Wtanzania kwa ujumla kutoyumba kwa kuwa Watanzania walio wengi bado wanakipenda Chama.

Ushindi wa mwaka huu wala si wa kimbunga ni wa Tsunami, watapiga kelele sana, watakuja na propaganda nyingi sana, lakini ushindi wa CCM ni lazima. Ni lazima tupate ushindi wa rais, wabunge, wawakilishi na madiwani,” alisema. 
 
Alisema walikuwa watu 42, wakati wakiomba kuteuliwa na chama hivi sasa, CCM ina kundi moja tu la ushindi.

“Hako ka tawi kamoja ndio kakameguka kwenda uko mbali, mti ambao unataka upate mbao zake nzuri matawi kudondoka chini ni vizuri ili upate mbao safi.
 
 “Lakini baada ya kudondoka hilo ni jambo la kawaida kwa chama kikubwa kama CCM.

"Hata ukiangalia tangu enzi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wapo waliotoka wako akina Kambona walitoka na wengine walifukuzwa na wengine walijua watafukuzwa wakakimbia wenyewe kabla ya kufukuzwa kama hao,” alisema.

Alisema iwapo atachaguliwa kuongoza dola atapenda awe mtumishi wa watu, asiyekuwa na majivuno ili aweze kuwatumikia wananchi na atimize matarajio yao.
 
 Dk Magufuli alisema wakati wa kampeni ukifika zitafanyika za kistaarabu na kisayansi na kwamba zitakuwa za shina kwa shina, tawi kwa tawi, kata kwa kata, jimbo kwa jimbo, wilaya, mkoa na taifa.

Aliwataka wana-CCM wasimame imara kwani wananchi wengi wanakipenda Chama.
 
 Dk Magufuli akizungumzia uzoefu wake ndani ya CCM, alisema alikuwa mbunge katika kipindi chake cha miaka 20, ambapo vipindi viwli alipita bila kupingwa na alikuwa waziri kwa miaka 20 katika wizara mbalimbali.

Alisema anaifahamu vizuri Mtwara, Tanzania, CCM na kero za Watanzania anazifahamu vya kutosha hivyo akipewa nafasi watashudia wenyewe kasi ya utendaji kwa maendeleo ya taifa.
 
 “Nilichaguliwa na mkutano mkuu kutoka kila kona ya nchi kwa asilimia 87, wale walionichagua waliwakishia Watanzania wote. Niwahakikishie kuwa mwaka huu, tutashinda zaidi,” alisema.
Aliwataka wana-CCM katika umoja wao kutulia na kutoyumbishwa na maneno ya porojo kwa kuwa chama kinajiuliza kwa kile walichofanya kwa wananchi na si maneno matamu bila vitendo.

“Chama nakifahamu, shida za wana-CCM nazifahamu, matarajio yao nayafahamu, shida za wananchi nazifahamu hivyo kama nitachaguliwa nitawatumikia kwa uadilifu mkubwa ili kuwaletea maendeleo,” alisema.

Sunday, August 9, 2015

BENKI YA POSTA TANZANIA, YASAIDIA SHULE ZA MSINGI WILAYANI ILEJE MKOANI MBEYA‏


  

Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mmbene, (wapili kushoto), akipeana mikono na Meneja msaidizi wa Benki ya Posta Tanzania, TPB, tawi la Tunduma, Teddy Msanzi, wakati wa hafla ya kukabidhi madawati yaliyotolewa kama msaada na benki hiyo, kusaidia shule mbili za msingi wilayani Ileje, mkoa wa Mbeya, hivi karibuni


Benki ya Posta Tanzania (TPB) kupitia tawi lake la Tunduma, imetoa msaada wa madawati 100 yenye thamani ya shilingi Milioni Tatu kwa shule mbili za Msingi zilizopo Wilayani Ileje, mkoani Mbeya.
Akikabidhi madawati hayo kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Janeth Mbene kwenye hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika Wilayani humo hivi karibuni, Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Tunduma Teddy Msanzi alisema kuwa,  Benki yake iliguswa sana na suala la uhaba wa madawati kwa wanafunzi wa Wilaya hiyo na kuona ni muhimu kusaidia.
“Benki ya Posta inatambua umuhimu wa elimu bora kwa ajili ya kujenga kizazi bora cha baadae. Ni vigumu kutoa elimu bora katika mazingira magumu ya wanafunzi kukaa chini madarasani.Ni vema wanafunzi wetu wakawekewa mazingira mazuri ya kupata elimu, ikiwemo madawati. Hivyo basi sisi Benki ya Posta tunatoa madawati haya 100 ili kupunguza tatizo hili.” Alifafanua Teddy.
Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi ya elimu wilaya Ileje, Wilaya hiyo ina jumla ya wanafunzi 28,488 wa shule za Msingi , lakini idadi ya madawatii ni 10,028, na kufanya idadi ya madawati yanayohitajika kuwa 4,116.
Akitoa shukrani zake kwa niaba ya shule za Wilaya ya Ileje, Mhe. Janeth Mbene aliishukuru Benki ya Posta kwa msaada huo ambao alisema ni mkombozi kwa wanafunzi waliokuwa wakikaa chini kwa muda mrefu. Alitumia fursa hiyo pia kuziomba taasisi nyingine ziguswe na tatizo lao na ziweze kuwasaidia ili waweze kuondokana na changamoto hiyo.


 Naibu Waziri Mmbene, akiwa na maafisa wa benki hiyo, tawi la Tunduma
 Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene akimkabidhi katibu wa CCM Wilaya ya Ileje Hamida Mbogo madawati ya kwa ajili ya shule za sekondari na msingi wilayani ileje ambayo yametolewa na benki Posta Tawi la Tunduma.

Saturday, August 8, 2015

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA KUHITIMISHA SIKU YA NANE NANE JIJINI MBEYA


 Hawa ni watu ambao wameweza kufika katika viwanja vya John Mwakangale kwa ajili ya kujionea mambo mbalimbali Nanenane
 Baadhi ya wanafunzi walionekana wakiwa kaika viwanja hivyo kwa ajili ya kujifunza mbalimbali yahusuyo Kilimo, ufugaji na Mengine mengiiiii....
 Wafanya Biashara nao hawakuwa mbali, kuumia fursa kupitia msimu wa nane nane.
 Uuzaji wa Mitumba ni miongoni mwa shughuli zinazofanywa katika viwanja vya nane nane 
 Wengine hao wanaondoka

Thursday, July 30, 2015

PICHA: Lowassa Achukua Fomu ya Urais CHADEMA

LOWASA (1)


Edward Lowassa akionesha fomu ya kuwania urais aliyokabidhiwa leo Makao makuu ya Chadema,D ar.
Umati wa watu waliojitokeza kumpokea Lowassa wakati akichukua fomu ya urais kupitia Chadema.
CLJ5hSGWoAACCU3CLJ8fhkW8AA6IKB
…Akisaini katika kitabu cha wageni.
CLJ9y4iWEAAZWy7CLJ52JsWwAA--Yc
Mnadhimu Mkuu kambi rasmi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu akitoa yake machache.
Lowassa akiwasiri kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Chadema, Dar leo.
CLKRw2sWcAAzeL9
mbowe na lowassa
Baada ya kuchukua fomu.
Mwenyekiti wa Chadema (kushoto) Mhe. Freeman Mbowe Mhe. Edward Lowassa (katikati) wakati wa zoezi la kuchukua fomu lililofanyika leo Makao Makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar .
LOWASA (2)
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiwa katika meza kuu ya Chadema.
 **
WAZIRI MKUU wa zamani, Mhe. Edward Lowassa hivi punde amechukua fomu ya kuwania nafasi ya urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 
Lowassa amekabidhiwa fomu hiyo na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kwenye ofisi za Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 
Lowassa alijiunga rasmi na Chadema juzi akitokea CCM baada ya kuondolewa kwenye mchakato wa kuwa mgombea urais wa chama hicho akidai kuwa jina lake liliondolewa kwa mizengwe.

No comments:

Post a Comment