Tuesday, June 23, 2015
Polisi Iringa yakamata DVD za Mafunzo ya kigaidi
Jeshi
la polisi mkoani Iringa limekamata mikanda ya DVD yenye mafunzo ya
kijeshi yanayohusiana na kikundi cha ugaidi cha Al shaabab cha nchini
Somalia zilizokuwa zikitumika na watoto wa mitaani wanaodaiwa kuwa
walikuwa wakichukua mafunzo kwakutumia DVD hizo.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Iringa ACP Ramadhan Mungi ametoa taarifa hiyo mbele
ya waandishi wa habari akieleza kuwa mikanda hiyo iliyokuwa ikitumiwa na
vijana hao wanne wenye umri kati ya miaka 12 na 16 inaonesha ukatili na
mauaji yanayodaiwa kufanywa na kikundi cha kigaidi cha Al
shaabab.Mikanda hiyo walikuwa wakiitazama kwa kutumia kompyuta mpakato
yaani laptop.
Aidha
kamanda Mungi amesema pamoja na mikanda hiyo ya DVD pia jeshi hilo
limekamata watu wawili wanaojihusisha na biashara ya bangi wakiwa na
magunia matatu ya bangi katika harakati za kufunga bangi hiyo kwenye
vifurushi vidogo tayari kuisambaza kwa wateja wao.
Mungi
ameongeza kuwa kamata kamata hiyo iliyofanywa na jeshi hilo mkoa wa
Iringa pia imekamata nguzo 35 za umeme za shirika la umeme nchini
TANESCO, nyaya za kusambaza umeme na vifaa vingine zikiwa zimehifadhiwa
kwa watu binafsi wawili ambao hakuwataja majina kwa sababu za
kiupelelezi.
MATUKIO KATIKA PICHA : MA ELFU WAMPOKEA LOWASA MBEYA JANA APATA WADHAMIMI 53,156 SHUHUDIA.

Umati
wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, wakiwa wamemzunguka,
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh.
Edward Lowassa (katikati), wakati alipowasili kwenye Ofisi za CCM Mkoa
wa Mbeya jana Juni 19, 2015, kukabidhiwa fomu zitakazomuwezesha kupata
ridhaa ya Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 25, 2015. Mbeya wamevunja rekodi udhamini kwa Mh.
Lowassa ya mikoa yote aliyopita, amepata wadhamini 53,156 kwa mkoa wa
Mbeya pekee.

Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akipunga mkono kwa Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa
wa Mbeya, waliofurika kwa wingi wao kwenye Uwanja wa Ofisi za CCM Mkoa
wa Mbeya, wakati alipowasili kwenye Ofisi hizo leo Juni 19, 2015, tayari
kwa kupokea fomu za WanaCCM 53,156 wanaliomdhamini ili apate ridhaa ya
Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25, 2015.


Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akizungumza machache na kutoa shukrani kwa WanaCCM na Wananchi
wa Mkoa wa Mbeya waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Ofisi za CCM
Mkoa wa Mbeya, leo Juni 19, 2015.

Furaha
ya Mh. Edward Lowassa kwa wanaCCM na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, hata
haikujificha pale alipata mapokezi makubwa ambayo hata yeye
hakuyategemea.

Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akipokea fomu za WanaCCM zaidi ya elfu tisa wa Wilaya ya Mbeya
Vijijini kutoka kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mary Kalinze.


Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, kwenye mji Mdogo wa Mbalizi wakati aliposimama kuwasalimia.

Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akisalimiana na Kijana Mwenye ulemavu, Ernest Mhagama aliekuja
kumpokea katika Uwanja wa Ndege Songwe, Jijini Mbeya jana Juni 19, 2015.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akitoka nje ya Uwanja wa Ndege wa Songwe na kulakiwa na umati wa
WanaCCM wa Mkoa wa Mbeya.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwapungia wanaCCM wa Mkoa wa Mbeya.
Shangwe kwa wanaCCM wa Mji wa Mbalizi, Mbeya Vijijini.
Mh. Lowassa akiteta jambo na Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya Vijijini.
Umati wa wanaCCM wa Mji wa Mbalizi jijini Mbeya.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akipokea fomu za WanaCCM zaidi ya elfu tisa wa Wilaya ya Mbeya
Vijijini kutoka kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mary Kalinze.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, kwenye mji Mdogo wa Mbalizi wakati aliposimama kuwasalimia.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akiwasalimia wanaCCM na Wananchi wa Mji wa Mbalizi jijini Mbeya
waliojitokeza kumlaki.
JOHN MWAMBIGIJA A.K.A (MZEE WA UPAKO) ATIKISA MJI WA TUKUYU WAKATI AKIRUDISHA FOMU YA UBUNGE, MAELFU YA WATU WAJITOKEZA NA MAGARI, PIKIPIKI WASABABISHA BARABARA YA K/ROAD KUFUNGWA KWA MUDA.
Hizi ni Ofisi za Chadema Jimbo la Rungwe Magharibi Tukuyu Mjini.
Huyu Ndio John D. Mwambigija Mtiania Ubunge jimbo la Rungwe Magharibi kwa
Tiketi ya Chadema.
Jinsi wananchi wa Rungwe walivyojitokeza kwa wingi kumuunga mkono Mtiania John Mwambigija wakati anarudisha Fomu.
John Mwambigija Katikakati akiongozana na wananchi kuelekea katika Ofisi za Jimbo la Rungwe Magharibi.
Mwenyekiti wa jimbo la Rungwe Magharibi, Juma Kibo akipokea fomu kwa mtiania John Mwambigija.
Red Briged wakihakikisha Ulinzi na usalama Unazingatiwa.
Mwenyekiti wa Jimbo Juma kibo akiwashukuru wananchi waliomsindikiza
John Mwambigija wakati wa kurudisha Fomu.
Mtiania John Mwambigija akizungumza neno la shukrani kwa wananchi waliomsindikiza kurudisha fomu.
............................................................................
IMEELEZWA kuwa umati mkubwa uliofurika kumsindikiza
kurudisha fomu ya ubunge wa jimbo la Rungwe Magharibi John Mwambigija (CHADEMA)
kutairahisishia kamati tendaji kufanya maamuzi sahihi katika kumpata mgombea
anayekubarika.
kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa jimbo hilo Juma
kibo wakati akiwashukuru maelfu ya wananchi waliojitokeza kumsindikiza mtia nia
huyo wakiwa na magari zaidi ya hamsini na pikipiki mia mbili na kupelekea
makada wa CCM kushikwa na mshangao.
alisema zaidi ya watia nia 24 waliochukua fomu ni mtia nia
mmoja pekee ndiyo aliyerejesha fomu saa tisa alasiri ya tarehe 22/06/2015,na
kuwataka wananchi kufanya hivyo kwa watia nia wengine ili kumpata mgombea
atakayepeperusha bendera katika uchaguzi mkuu wa Oktober mwaka huu.
John Mwambigija (Mzee wa upako) mbali na kuwapongeza
wananchi na makada wa chama hicho waliojitokeza kwa wingi kumsindikiza
kurudisha fomu,amesema pindi chama kitakapompitisha na kutwaa ubunge
atahakikisha anaziondoa changamoto zilizopo na kuleta usawa kwa wana Rungwe.
Alisema wilaya ya Rungwe inavyanzo vingi vya mapato ikiwemo
viwanda, Chai na gesi asilia inayovunwa na kupelekwa Dar es saalam lakini
wananchi wa Rungwe wamekuwa ni masikini wa kutupwa kutokana na uongozi mbovu wa
Serikali ya Chama cha Mapinduzi.
''Tumekuwa na wabunge maprofesa Mark Mwandosya na David
Mwakyusa kwa muda wa miaka kumi na tano lakini wamekuwa ni mizigo wasio kuwa na
huruma kwa wananchi waliowachagua nikiwa mbunge nitareta mabadiriko''alisema.
Mwambigija aliyebatizwa Majina Kama
waziri mkuu wa Mbeya na Yohana mbatizaji, alisema akiwa mbunge hatahamia Dar es
salaam kama ilivyo kwa wabunge wa chama cha mapinduzi na kuwa atahakikisha
anaboresha sekta zote zilizodhorota.
Na Rungwe Yetu
Na Rungwe Yetu
Subscribe to:
Posts (Atom)