Tuesday, June 23, 2015

Mkutano mkuu wa ACT mkoa wa mbeya ktk viwanja vya rwanda nzovwe.

       Mkutano ulihutubiwa na kiongozi wa chama cha Wazalendo ACT  katika viwanja vya Nzovwe mbeya huku Mh Zito Kabwe akiahidi kuwa (Pesa zangu za halali za kiinua mgongo za ubunge zote ntazipereke shule ya walemavu wa ngozi.albino SHINYANGA.) alisema Zitto Kabwe




Polisi Iringa yakamata DVD za Mafunzo ya kigaidi




Jeshi la polisi mkoani Iringa limekamata mikanda ya DVD yenye mafunzo ya kijeshi yanayohusiana na kikundi cha ugaidi cha Al shaabab cha nchini Somalia zilizokuwa zikitumika na watoto wa mitaani wanaodaiwa kuwa walikuwa wakichukua mafunzo kwakutumia DVD hizo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa ACP Ramadhan Mungi ametoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari akieleza kuwa mikanda hiyo iliyokuwa ikitumiwa na vijana hao wanne wenye umri kati ya miaka 12 na 16 inaonesha ukatili na mauaji yanayodaiwa kufanywa na kikundi cha kigaidi cha Al shaabab.Mikanda hiyo walikuwa wakiitazama kwa kutumia kompyuta mpakato yaani laptop.

Aidha kamanda Mungi amesema pamoja na mikanda hiyo ya DVD pia jeshi hilo limekamata watu wawili wanaojihusisha na biashara ya bangi wakiwa na magunia matatu ya bangi katika harakati za kufunga bangi hiyo kwenye vifurushi vidogo tayari kuisambaza kwa wateja wao.

Mungi ameongeza kuwa kamata kamata hiyo iliyofanywa na jeshi hilo mkoa wa Iringa pia imekamata nguzo 35 za umeme za shirika la umeme nchini TANESCO, nyaya za kusambaza umeme na vifaa vingine zikiwa zimehifadhiwa kwa watu binafsi wawili ambao hakuwataja majina kwa sababu za kiupelelezi.

MATUKIO KATIKA PICHA : MA ELFU WAMPOKEA LOWASA MBEYA JANA APATA WADHAMIMI 53,156 SHUHUDIA.




Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, wakiwa wamemzunguka, Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa (katikati), wakati alipowasili kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya jana Juni 19, 2015, kukabidhiwa fomu zitakazomuwezesha kupata ridhaa ya Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mbeya wamevunja rekodi udhamini kwa Mh. Lowassa ya mikoa yote aliyopita, amepata wadhamini 53,156 kwa mkoa wa Mbeya pekee.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akipunga mkono kwa Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, waliofurika kwa wingi wao kwenye Uwanja wa Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya, wakati alipowasili kwenye Ofisi hizo leo Juni 19, 2015, tayari kwa kupokea fomu za WanaCCM 53,156 wanaliomdhamini ili apate ridhaa ya Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza machache na kutoa shukrani kwa WanaCCM na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya, leo Juni 19, 2015.
Furaha ya Mh. Edward Lowassa kwa wanaCCM na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, hata haikujificha pale alipata mapokezi makubwa ambayo hata yeye hakuyategemea.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akipokea fomu za WanaCCM zaidi ya elfu tisa wa Wilaya ya Mbeya Vijijini kutoka kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mary Kalinze.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, kwenye mji Mdogo wa Mbalizi wakati aliposimama kuwasalimia.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Kijana Mwenye ulemavu, Ernest Mhagama aliekuja kumpokea katika Uwanja wa Ndege Songwe, Jijini Mbeya jana Juni 19, 2015.


 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akitoka nje ya Uwanja wa Ndege wa Songwe na kulakiwa na umati wa WanaCCM wa Mkoa wa Mbeya.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.

 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwapungia wanaCCM wa Mkoa wa Mbeya.
 Shangwe kwa wanaCCM wa Mji wa Mbalizi, Mbeya Vijijini.
 Mh. Lowassa akiteta jambo na Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya Vijijini.
 Umati wa wanaCCM wa Mji wa Mbalizi jijini Mbeya.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akipokea fomu za WanaCCM zaidi ya elfu tisa wa Wilaya ya Mbeya Vijijini kutoka kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mary Kalinze.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, kwenye mji Mdogo wa Mbalizi wakati aliposimama kuwasalimia.
  Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwasalimia wanaCCM na Wananchi wa Mji wa Mbalizi jijini Mbeya waliojitokeza kumlaki.

JOHN MWAMBIGIJA A.K.A (MZEE WA UPAKO) ATIKISA MJI WA TUKUYU WAKATI AKIRUDISHA FOMU YA UBUNGE, MAELFU YA WATU WAJITOKEZA NA MAGARI, PIKIPIKI WASABABISHA BARABARA YA K/ROAD KUFUNGWA KWA MUDA.

Hizi ni Ofisi za Chadema Jimbo la Rungwe Magharibi Tukuyu Mjini.

Huyu Ndio John D. Mwambigija Mtiania Ubunge jimbo la Rungwe Magharibi kwa 
Tiketi ya Chadema.
Jinsi wananchi wa Rungwe walivyojitokeza kwa wingi kumuunga mkono Mtiania John Mwambigija wakati anarudisha Fomu.
 John Mwambigija Katikakati akiongozana na wananchi kuelekea katika Ofisi za Jimbo la Rungwe Magharibi.
 Mwenyekiti wa jimbo la Rungwe Magharibi, Juma Kibo akipokea fomu kwa mtiania John Mwambigija.

                                         Wananchi wakiwa Nje wakimsubiri John Mwambigija.

 Red Briged wakihakikisha Ulinzi na usalama Unazingatiwa.


                Mwenyekiti wa Jimbo Juma kibo akiwashukuru wananchi waliomsindikiza 
                            John  Mwambigija wakati wa kurudisha Fomu.
  
Mtiania John Mwambigija akizungumza neno la shukrani kwa wananchi waliomsindikiza kurudisha fomu.
............................................................................


IMEELEZWA kuwa umati mkubwa uliofurika kumsindikiza kurudisha fomu ya ubunge wa jimbo la Rungwe Magharibi John Mwambigija (CHADEMA) kutairahisishia kamati tendaji kufanya maamuzi sahihi katika kumpata mgombea anayekubarika.
kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa jimbo hilo Juma kibo wakati akiwashukuru maelfu ya wananchi waliojitokeza kumsindikiza mtia nia huyo wakiwa na magari zaidi ya hamsini na pikipiki mia mbili na kupelekea makada wa CCM kushikwa na mshangao.
alisema zaidi ya watia nia 24 waliochukua fomu ni mtia nia mmoja pekee ndiyo aliyerejesha fomu saa tisa alasiri ya tarehe 22/06/2015,na kuwataka wananchi kufanya hivyo kwa watia nia wengine ili kumpata mgombea atakayepeperusha bendera katika uchaguzi mkuu wa Oktober mwaka huu.
John Mwambigija (Mzee wa upako) mbali na kuwapongeza wananchi na makada wa chama hicho waliojitokeza kwa wingi kumsindikiza kurudisha fomu,amesema pindi chama kitakapompitisha na kutwaa ubunge atahakikisha anaziondoa changamoto zilizopo na kuleta usawa kwa wana Rungwe.
Alisema wilaya ya Rungwe inavyanzo vingi vya mapato ikiwemo viwanda, Chai na gesi asilia inayovunwa na kupelekwa Dar es saalam lakini wananchi wa Rungwe wamekuwa ni masikini wa kutupwa kutokana na uongozi mbovu wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi.
''Tumekuwa na wabunge maprofesa Mark Mwandosya na David Mwakyusa kwa muda wa miaka kumi na tano lakini wamekuwa ni mizigo wasio kuwa na huruma kwa wananchi waliowachagua nikiwa mbunge nitareta mabadiriko''alisema.
Mwambigija aliyebatizwa Majina Kama waziri mkuu wa Mbeya na Yohana mbatizaji, alisema akiwa mbunge hatahamia Dar es salaam kama ilivyo kwa wabunge wa chama cha mapinduzi na kuwa atahakikisha anaboresha sekta zote zilizodhorota.

Na Rungwe Yetu