Friday, August 14, 2015

Magufuli Aahidi Ushindi wa Tsunami CCM......Asema Wapinzani Wataishia Kupiga Kelele Tu, Mwigulu Nchemba Naye Apigilia Msumari wa 'Moto'



MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli, amewahakikishia wana-CCM na Watanzaia kwa ujumla kuwa mwaka huu, chama kitapata ushindi wa Tsunami na si wa kishindo wala kimbunga.

Dk Magufuli alisema hayo nje ya ofisi ya chama hicho mkoani Mtwara juzi alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama hicho ambapo alisisitiza kuwa wapinzani watapiga kelele sana, wataongea sana lakini ushindi kwa CCM ni lazima na upo pale pale.

Alisema ushindi huo unatokana na matawi yaliyoanguka ndani ya chama na kuhama na kwamba watu hao wameiacha CCM ikiwa safi na salama zaidi. 
 
Alisema watu hao walikuwa wakitumia fedha nyingi kurubuni watu wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM ambapo chama kiliwakata na kukimbilia vyama vingine vya upinzani.

Aliwataka wana-CCM wasikatishwe tamaa na watu wa aina hiyo na badala yake washikamane, wawe kitu kimoja na kwamba mwaka huu, chama kitafanya kampeni za kisayansi. 
 
Aidha, Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba alisema ni kazi rahisi kumnadi Dk Magufuli kutokana na vigezo na sifa alizonazo.

Mwigulu, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, alisema walioshindwa kwenye mchakato wa kura za maoni na kuhama ndani ya chama, hivi sasa wanahaha kutafuta urais wenyewe ambapo wanatoa mpaka hela ili kutafuta uongozi, lakini wataumbuka mapema.

Akizungumza na mamia ya wana-CCM waliojitokeza kumpokea katika hiyo ofisi ya chama ambapo alifika kwa ajili ya kuwasalimia na kuwashukuru kwa kumchagua kuwa mgombea na kumdhamini, Dk Magufuli aliwataka makada hao na Wtanzania kwa ujumla kutoyumba kwa kuwa Watanzania walio wengi bado wanakipenda Chama.

Ushindi wa mwaka huu wala si wa kimbunga ni wa Tsunami, watapiga kelele sana, watakuja na propaganda nyingi sana, lakini ushindi wa CCM ni lazima. Ni lazima tupate ushindi wa rais, wabunge, wawakilishi na madiwani,” alisema. 
 
Alisema walikuwa watu 42, wakati wakiomba kuteuliwa na chama hivi sasa, CCM ina kundi moja tu la ushindi.

“Hako ka tawi kamoja ndio kakameguka kwenda uko mbali, mti ambao unataka upate mbao zake nzuri matawi kudondoka chini ni vizuri ili upate mbao safi.
 
 “Lakini baada ya kudondoka hilo ni jambo la kawaida kwa chama kikubwa kama CCM.

"Hata ukiangalia tangu enzi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wapo waliotoka wako akina Kambona walitoka na wengine walifukuzwa na wengine walijua watafukuzwa wakakimbia wenyewe kabla ya kufukuzwa kama hao,” alisema.

Alisema iwapo atachaguliwa kuongoza dola atapenda awe mtumishi wa watu, asiyekuwa na majivuno ili aweze kuwatumikia wananchi na atimize matarajio yao.
 
 Dk Magufuli alisema wakati wa kampeni ukifika zitafanyika za kistaarabu na kisayansi na kwamba zitakuwa za shina kwa shina, tawi kwa tawi, kata kwa kata, jimbo kwa jimbo, wilaya, mkoa na taifa.

Aliwataka wana-CCM wasimame imara kwani wananchi wengi wanakipenda Chama.
 
 Dk Magufuli akizungumzia uzoefu wake ndani ya CCM, alisema alikuwa mbunge katika kipindi chake cha miaka 20, ambapo vipindi viwli alipita bila kupingwa na alikuwa waziri kwa miaka 20 katika wizara mbalimbali.

Alisema anaifahamu vizuri Mtwara, Tanzania, CCM na kero za Watanzania anazifahamu vya kutosha hivyo akipewa nafasi watashudia wenyewe kasi ya utendaji kwa maendeleo ya taifa.
 
 “Nilichaguliwa na mkutano mkuu kutoka kila kona ya nchi kwa asilimia 87, wale walionichagua waliwakishia Watanzania wote. Niwahakikishie kuwa mwaka huu, tutashinda zaidi,” alisema.
Aliwataka wana-CCM katika umoja wao kutulia na kutoyumbishwa na maneno ya porojo kwa kuwa chama kinajiuliza kwa kile walichofanya kwa wananchi na si maneno matamu bila vitendo.

“Chama nakifahamu, shida za wana-CCM nazifahamu, matarajio yao nayafahamu, shida za wananchi nazifahamu hivyo kama nitachaguliwa nitawatumikia kwa uadilifu mkubwa ili kuwaletea maendeleo,” alisema.

Sunday, August 9, 2015

BENKI YA POSTA TANZANIA, YASAIDIA SHULE ZA MSINGI WILAYANI ILEJE MKOANI MBEYA‏


  

Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mmbene, (wapili kushoto), akipeana mikono na Meneja msaidizi wa Benki ya Posta Tanzania, TPB, tawi la Tunduma, Teddy Msanzi, wakati wa hafla ya kukabidhi madawati yaliyotolewa kama msaada na benki hiyo, kusaidia shule mbili za msingi wilayani Ileje, mkoa wa Mbeya, hivi karibuni


Benki ya Posta Tanzania (TPB) kupitia tawi lake la Tunduma, imetoa msaada wa madawati 100 yenye thamani ya shilingi Milioni Tatu kwa shule mbili za Msingi zilizopo Wilayani Ileje, mkoani Mbeya.
Akikabidhi madawati hayo kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Janeth Mbene kwenye hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika Wilayani humo hivi karibuni, Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Tunduma Teddy Msanzi alisema kuwa,  Benki yake iliguswa sana na suala la uhaba wa madawati kwa wanafunzi wa Wilaya hiyo na kuona ni muhimu kusaidia.
“Benki ya Posta inatambua umuhimu wa elimu bora kwa ajili ya kujenga kizazi bora cha baadae. Ni vigumu kutoa elimu bora katika mazingira magumu ya wanafunzi kukaa chini madarasani.Ni vema wanafunzi wetu wakawekewa mazingira mazuri ya kupata elimu, ikiwemo madawati. Hivyo basi sisi Benki ya Posta tunatoa madawati haya 100 ili kupunguza tatizo hili.” Alifafanua Teddy.
Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi ya elimu wilaya Ileje, Wilaya hiyo ina jumla ya wanafunzi 28,488 wa shule za Msingi , lakini idadi ya madawatii ni 10,028, na kufanya idadi ya madawati yanayohitajika kuwa 4,116.
Akitoa shukrani zake kwa niaba ya shule za Wilaya ya Ileje, Mhe. Janeth Mbene aliishukuru Benki ya Posta kwa msaada huo ambao alisema ni mkombozi kwa wanafunzi waliokuwa wakikaa chini kwa muda mrefu. Alitumia fursa hiyo pia kuziomba taasisi nyingine ziguswe na tatizo lao na ziweze kuwasaidia ili waweze kuondokana na changamoto hiyo.


 Naibu Waziri Mmbene, akiwa na maafisa wa benki hiyo, tawi la Tunduma
 Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene akimkabidhi katibu wa CCM Wilaya ya Ileje Hamida Mbogo madawati ya kwa ajili ya shule za sekondari na msingi wilayani ileje ambayo yametolewa na benki Posta Tawi la Tunduma.

Saturday, August 8, 2015

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA KUHITIMISHA SIKU YA NANE NANE JIJINI MBEYA


 Hawa ni watu ambao wameweza kufika katika viwanja vya John Mwakangale kwa ajili ya kujionea mambo mbalimbali Nanenane
 Baadhi ya wanafunzi walionekana wakiwa kaika viwanja hivyo kwa ajili ya kujifunza mbalimbali yahusuyo Kilimo, ufugaji na Mengine mengiiiii....
 Wafanya Biashara nao hawakuwa mbali, kuumia fursa kupitia msimu wa nane nane.
 Uuzaji wa Mitumba ni miongoni mwa shughuli zinazofanywa katika viwanja vya nane nane 
 Wengine hao wanaondoka

Thursday, July 30, 2015

PICHA: Lowassa Achukua Fomu ya Urais CHADEMA

LOWASA (1)


Edward Lowassa akionesha fomu ya kuwania urais aliyokabidhiwa leo Makao makuu ya Chadema,D ar.
Umati wa watu waliojitokeza kumpokea Lowassa wakati akichukua fomu ya urais kupitia Chadema.
CLJ5hSGWoAACCU3CLJ8fhkW8AA6IKB
…Akisaini katika kitabu cha wageni.
CLJ9y4iWEAAZWy7CLJ52JsWwAA--Yc
Mnadhimu Mkuu kambi rasmi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu akitoa yake machache.
Lowassa akiwasiri kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Chadema, Dar leo.
CLKRw2sWcAAzeL9
mbowe na lowassa
Baada ya kuchukua fomu.
Mwenyekiti wa Chadema (kushoto) Mhe. Freeman Mbowe Mhe. Edward Lowassa (katikati) wakati wa zoezi la kuchukua fomu lililofanyika leo Makao Makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar .
LOWASA (2)
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiwa katika meza kuu ya Chadema.
 **
WAZIRI MKUU wa zamani, Mhe. Edward Lowassa hivi punde amechukua fomu ya kuwania nafasi ya urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 
Lowassa amekabidhiwa fomu hiyo na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kwenye ofisi za Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 
Lowassa alijiunga rasmi na Chadema juzi akitokea CCM baada ya kuondolewa kwenye mchakato wa kuwa mgombea urais wa chama hicho akidai kuwa jina lake liliondolewa kwa mizengwe.

Dk Slaa aikana twitter inayomzushia mazito


Wakati kukiwa na taarifa zinazosambaa mtandaoni zikimuhusisha Dk Willibrod Slaa na akaunti ambayo imekuwa ikitoa msimamo wake wa kujitenga na shughuli za siasa pamoja na Ukawa, katibu huyo mkuu wa Chadema amekanusha taarifa hizo akisema hajawahi kuwa na akaunti ya twitter.
 
Dk Slaa, aliyekuwa anatajwa kuwa mgombea urais wa Chadema, hajaonekana hadharani katika matukio makubwa ya kichama tangu Chadema na Ukawa walipomkaribisha waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kumteua kuwa mgombea urais anayeungwa mkono na vyama vinne vinavyounda umoja huo.

Mara ya mwisho kuonekana kwenye shughuli za chama hicho ni katika kikao cha Kamati Kuu wakati Lowassa alikaribishwa kufanya majadiliano na kujibu hoja za wajumbe.

Lakini baada ya hapo Dk Slaa hakuonekana wakati wa kutambulishwa kwa Lowassa kwa waandishi wa habari, tukio la kuchukua na kurudisha fomu za urais ndani ya chama na tukio la juzi la kuchukua fomu za urais kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Wakati hayo yakiendelea, kuna akaunti ya twitter yenye jina la “Dr Willibrord Slaa” ambayo imekuwa ikitoa kauli mfululizo zikiwa na ujumbe mbalimbali unaoendana na mazingira aliyomo sasa mwanasiasa huyo.

 Agosti 10, kulitumwa ujumbe zaidi mara 10, mmojawapo ukijaribu kuwaaminisha watu kuwa hiyo ni akaunti halisi ya Dk Slaa.

“Ndugu zangu Watanzania, hii ni akaunti yangu rasmi, bila shaka yoyote na naomba ninachoandika hapa kifikishwe kwa Watanzania popote walipo,” unasema ujumbe huo.

Taarifa nyingine zilizotumwa kwenye akaunti hiyo ya twitter ni pamoja na ile iliyoeleza kuwa   Dk Slaa ameomba ulinzi kutoka nchi na mashirika ya kimataifa na atazungumza kupitia runinga na redio pindi atakapopata ulinzi.

Akizungumzia sakata  hili jana, Dk Slaa alisema hajawahi kutuma taarifa yoyote kwenye mitandao ya kijamii.

“Sijawahi ku-operate (kuendesha) kitu chochote kwenye akaunti ya twitter, sina akaunti kama hiyo,” alisema Dk Slaa.

Mbali na kukanusha kumiliki na kuendesha akaunti hiyo, Dk Slaa alirudia kauli yake ya wiki iliyopita kuwa atatoa msimamo wake muda muafaka utakapofika, baada ya kuulizwa swali kuhusu hatma yake ndani ya Chadema na kisiasa kwa ujumla.

“Subira yavuta heri, sasa ili uipate hiyo heri unatakiwa kuvumilia. Kwa hiyo wakati ukifika nitazungumza tu na Watanzania,” alisema.

Alipoulizwa ni wapi alipo kwa sasa, alisema yupo Dar es Salaam anapumzika, lakini akasisitiza kuwa ipo siku ataweka wazi mustakabali wake kisiasa.

Dk Slaa alisema yeye na mke wake Josephine Mushumbusi wanatarajia kusafiri kwenda nje ya nchi katika siku chache zijazo, ingawa hakuweka wazi nchi anayotarajia kuitembelea, lakini akasema atarejea baada ya wiki moja.

TUKIO LA KUSIKITISHA : RUNGWE AUAWA KINYAMA NA KUTUPWA KADO YA BARABARA




Tukio hilo limetokea wilayani rungwe mkoani Mbeya kata ya Katumba. Marehemu anasadikika kuwa ni mkazi wa Wilayani Ileje Mkoani Mbeya.
Pia inasemekana kuwa marehemu ametupwa sehemu hiyo usiku wa kuamkia leo na watu wasiosemekana  kwa kutumia Usafiri wa bodaboda.
                                     Picha zaidi.










Thursday, July 23, 2015

Ajali Mbaya ya Basi la Simiyu Express Yaua Watu Wengi Dodoma Usiku wa Kuamkia Leo


Taarifa kutoka mkoani Dodoma zinasema watu  zaidi  ya 10  wamefariki dunia usiku wa kuamkia leo , huku zaidi ya abiria 40 wakijeruhiwa vibaya baada ya basi la kampuni ya SIMIYU EXPRESS walilokua wakisafiria kutoka Mwanza kwenda DSM kupasuka tairi na kuacha njia na kugonga mbuyu na kisha kupinduka.
 
Taarifa zinasema ajali hiyo ni mbaya sana kuwahi kutokea mkoani Dodoma.Majeruhi wamekimbizwa katika Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma kwa ajili ya matibabu.

MFAHAM MGOMBEA WA UBUNGE KURA ZA MAONI MBEYA MJINI MCHAPAKAZ MPIGANAJI NDUGU SHADRACK MAKOMBE

Jumatano, 27 Mei 2015

MAAFISA SITA WA NGAZ YA JUU YA SHIRIKISHO LA KABUMBU ULIMWENGUN FIFA WAMEKAMATWA

Maafisa sita wa ngazi ya juu wa shirikisho la kabumbu ulimwenguni FIFA,wamekamatwa na maafisa wa vyombo vya sheria vya Uswisi hii leo mjini Zurich,siku mbili kabla ya mkutano mkuu wa shirikisho hilo.Maafisa hao wanakabiliwa na kitisho cha kuhamishiwa Marekani.Huko watakabiliwa na madai ya kuhusika na visa vya udanganyifu,ukandamizaji,na kubadilisha fedha kinyume cha sheria.Kwa mujibu wa idara ya sheria ya serikali kuu ya Uswisi,maafisa hao wa FIFA wanakabiliwa na tuhuma za kupokea rushwa ya mamilioni ya dola tangu mwaka 1990 kutoka vyombo vya habari za spoti na makampuni ya zana za spoti.Badala yake makampuni hayo yamepatiwa ruhusa ya kuripoti,kusimamia na kushughulikia masuala ya kibiashara katika michuano ya kabumbu nchini Marekani na Amerika ya kusini.Mwenyekiti wa FIFA,Joseph Blatter si miongoni mwa watuhumiwa. Bwana huyo mwenye umri wa miaka 79 atapigania kuchaguliwa upya ijumaaa ijayo kuliongoza shirikisho hilo la dimba ulimwenguni.

BENK YA MAENDELEO YA AFRICA INAANDAA MKUTANO.....

Benki ya maendeleo ya Africa, inaandaa mkutano wake wa kila mwaka huku ikiadhimisha miaka 50 tangu kuasisiwa kwake. Hapo kesho benki hiyo itamchagua rais wake mpya atakayechukua nafasi iliokuwa ikishikiliwa na Donald Kaberuka raia wa Rwanda. Je ni mafanikio ya aina gani yaliopatikana barani Africa tangu kuanzishwa kwa benki hiyo?

MNYAMA WA AJABU WAGUNDULIWA TANZANIA.....

Tanzania iliyobalikiwa
Mnyama wa ajabu agunduliwa Tanzania - "Tembomilia"
Kwa mara ya kwanza askari wa wanyamapori katika mbuga ya Serengeti nchini Tanzania wamemgundua mnyama huyu waliyempa jina la "Tembomilia" na wanasayansi wanasema ni mara ya kwanza kwa kiumbe cha aina hii kuonekana duniani. Hivi sasa walinzi hao wa wanyamapori na wanasayansi wanamuhifadhi mnyama huyu wa ajabu, ambaye wanasayansi tayari wamempa jina la kitaalamu la "Tembomilia Tanzanianicus". Jina lenyewe la "Tembomilia" linatokana na maneno ya Kiswahili "tembo" na "pundamilia". Tembomilia aliyegunduliwa sasa ni wa dume akiwa na umri unaokisiwa kuwa miaka miwili na uzito wa kilo 520.
Na sasa ikiwa umeamini habari hii, basi tumefanikiwa kukushika kwenye mzaha wa Aprili Mosi.

DIAMOND NA UTAJIRI WAKE WOTE ILA KAMWE HATAMFIKIA DAVIDO KWA UTAJIRI. HIZI NDO MALI ZA KIFAHARI ZA DAIVIDO. BOFYA HAPA

The Nigerian singer, who is undoubtedly one of the richest in his country, is living the high life. From private jets to fast cars and poshy residences, this dude is living the life. The BET winner, MTV-EMA and MOBO Nominee is known for his lavish spending stunts and occasional tweefs with his counterpart, Wiz Kid.
David Adedeji Adeleke as he is called by birth name, lives a trendy lifestyle and is one of the most sought for musicians in Africa.

Check out some the clothes, cars and homes he owns below:






WEMA SEPETU ATAZIMIA AKIZIONA PICHA HIZI ZA IDRIS AKIWA NA SAMANTHA WAKE>>>>.TEAM WEMA TU WAKOMENT

..



Jumamosi, 9 Mei 2015

FWATILIA MOMBO MUIMU KWA KUJUAA KIONGOZ BORA NA BORA KIONGOZ KWA KIJANA ALIYE TANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI SHEQ SHADRACK MAKOMBE

Nipe fursa
Katika mjadala huu,kumekuwepo na upotoshaji mkubwa wenye ni ovu ya kuchafua haiba za watu.
Dr.Slaa akiwa mwana ccm kwa umri wake wote wa ujana na kiongozi wa Tanu Youth League aliposhindwa uchaguzi wa kura ya maoni mwaka 1995 aliamua kuhamia Chadema na kumwacha Mkewe akiitumikia chadema lkn hakuwahi huitwa Msaliti.
Tundu Lissu alikuwa Mwana ccm kindakindaki na baadae kutimkia NCCR ambako nako hakudumu na kuhamia Chadema lkn hakuna aliemwita Msaliti.
Benson Kigaila alikuwa Kiongozi wa UDP na baadae kihamia chadema ambako sasa ni mkurugenzi wa Oparation na Mafunzo na anaitwa kamanda licha ya kuhama chama.
Lema alikuwa chama cha NCCR baadae akahama na Mrema kwenda TLP na baada ya kuona imekufa akatimkia chadema ,leo anaitwa kamanda na si Msaliti.
Mabere Marando alikuwa mwana ccm baadae akawa katibu mkuu wa NCCR mageuzi na hatimae akahamia Chadema ambako amewahi kuwa mwanasheria mkuu wa chama kabla hajatiliwa mashaka na kuondolewa haraka.leo ni kamanda na si Msaliti.
Prof.Abdallah Jumbe safari alikuwa kiongozi wa chama cha wananchi CUF na baadae akajiunga na chadema lkn hakuitwa msaliti licha ya kuwa alijiunga wakati CUF ikiwa chama kikuu cha upinzani nchini.
Orodha ni ndefu sana ....hao ni kwa uchache tu.
Sasa hoja yangu ni kuwa hivi karibuni kumeanzishwa Chama Kipya cha Alliance For Change and Transparency (ACT-Wazalendo)
Chama hiki kama vilivyo vyama vingine vilivyoanzishwa baada ya ccm,kinategemea kupata wanachama toka vyama mbalimbali na wale wasiokuwa na vyama.
Wapo walitoka ccm,ADC,CUF,NCCR-Mageuzi,n.k
Lkn hawa wakihamia ACT-husikii malalamiko(huenda wanatokea vyama vilivyokomaa kidemokrasia)
Kelele na maneno ya Usaliti hutolewa pake mwanachama anapohama toka chadema kwenda ACT.
Je kwanini CUF walitulia na kumtakia mausha mazuri ya kisiasa Prof Safari badala ya kuituhumu chadema?
Kwanini Ninyi hamjifunzi kwa waliotangulia kwenye siasa?
Hata wale waliohama ACT na kurudi chadema Mbona sisikii ACT wakilalamika?
Siasa ni kama Mpira,Mchezaji unaemtegemea anahamia kwa hasimu wako na bado haiwi mwisho wa Timu.
Rejea kadhia ta Van Persie kuhamia Man U,Tambwe Kuhamia Yanga,na Okwi kichezea Simba na baadae Yanga na sasa Simba tena.
Tuufunge Mjadala kwa kila chama kurudi kwenye malengo ya uanzishwaji wake.
Chadema fufueni M4C muendelee na mapambano kivyenu.
ACT-Wazalendo nao waendelee na Oparation zao za kuhakikisha nchi inarudi kwenye misingi ya kuasisiwa kwake.
CUF nao waendelee na kuhakikisha Tanzania inatoa haki sawa kwa wote n.k
Tunatofautiana Ideology japo focus ni kuondoa unyonyaji wa ccm.
Majangili,Wauza unga,Mafisadi na kila waovu wa nchi hii wananufaika na mgawanyiko wa Upinzani.
Foward ever,Backward Hahahahah daima huwa napenda sera za USA kwani kwao kiongozi bora ni yule aliye jikomboa kifikra na kiuchumi ndio kiongozi bora na si vinginevyo    WATANZANIA wanahitaji viongozi wanaokuja na solution na co viongozi wanaokuja na matatizo kama sehemu ya jamii