Tundu Lissu alikuwa Mwana ccm kindakindaki na baadae kutimkia NCCR
ambako nako hakudumu na kuhamia Chadema lkn hakuna aliemwita Msaliti.
Benson Kigaila alikuwa Kiongozi wa UDP na baadae kihamia chadema ambako
sasa ni mkurugenzi wa Oparation na Mafunzo na anaitwa kamanda licha ya
kuhama chama.
Lema alikuwa chama cha NCCR baadae akahama na Mrema kwenda TLP na baada
ya kuona imekufa akatimkia chadema ,leo anaitwa kamanda na si Msaliti.
Mabere Marando alikuwa mwana ccm baadae akawa katibu mkuu wa NCCR
mageuzi na hatimae akahamia Chadema ambako amewahi kuwa mwanasheria mkuu
wa chama kabla hajatiliwa mashaka na kuondolewa haraka.leo ni kamanda
na si Msaliti.
Prof.Abdallah Jumbe safari alikuwa kiongozi wa chama cha wananchi CUF na
baadae akajiunga na chadema lkn hakuitwa msaliti licha ya kuwa
alijiunga wakati CUF ikiwa chama kikuu cha upinzani nchini.
Orodha ni ndefu sana ....hao ni kwa uchache tu.
Sasa hoja yangu ni kuwa hivi karibuni kumeanzishwa Chama Kipya cha Alliance For Change and Transparency (ACT-Wazalendo)
Chama hiki kama vilivyo vyama vingine vilivyoanzishwa baada ya
ccm,kinategemea kupata wanachama toka vyama mbalimbali na wale wasiokuwa
na vyama.
Wapo walitoka ccm,ADC,CUF,NCCR-Mageuzi,n.k
Lkn hawa wakihamia ACT-husikii malalamiko(huenda wanatokea vyama vilivyokomaa kidemokrasia)
Kelele na maneno ya Usaliti hutolewa pake mwanachama anapohama toka chadema kwenda ACT.
Je kwanini CUF walitulia na kumtakia mausha mazuri ya kisiasa Prof Safari badala ya kuituhumu chadema?
Kwanini Ninyi hamjifunzi kwa waliotangulia kwenye siasa?
Hata wale waliohama ACT na kurudi chadema Mbona sisikii ACT wakilalamika?
Siasa ni kama Mpira,Mchezaji unaemtegemea anahamia kwa hasimu wako na bado haiwi mwisho wa Timu.
Rejea kadhia ta Van Persie kuhamia Man U,Tambwe Kuhamia Yanga,na Okwi kichezea Simba na baadae Yanga na sasa Simba tena.
Tuufunge Mjadala kwa kila chama kurudi kwenye malengo ya uanzishwaji wake.
Chadema fufueni M4C muendelee na mapambano kivyenu.
ACT-Wazalendo nao waendelee na Oparation zao za kuhakikisha nchi inarudi kwenye misingi ya kuasisiwa kwake.
CUF nao waendelee na kuhakikisha Tanzania inatoa haki sawa kwa wote n.k
Tunatofautiana Ideology japo focus ni kuondoa unyonyaji wa ccm.
Majangili,Wauza unga,Mafisadi na kila waovu wa nchi hii wananufaika na mgawanyiko wa Upinzani.